Orodha ya Hadithi

Hivi nisikuelezeni juu ya dhambi kubwa kuliko yote?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapo mpenda mtu ndugu yake amwambie kuwa anampenda.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Madhambi makubwa: Ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kuwaasi wazazi wawili na kuuwa nafsi, na kiapo cha uongo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenye kwenda mbio kuwasaidia wajane na masikini, ni kama mwenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
"Jiepusheni na mambo saba yenye kuangamiza, wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni yapi hayo? Akasema: Ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu, na uchawi, na kuuwa nafsi aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu ispokuwa kwa haki, na kula riba, na kula mali ya yatima, na kukimbia siku ya mapambano, na kuwazulia machafu wanawake waumini wenye kujihifadhi wenye kujizuia na machafu".
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mimi nimejitosheleza na washirika juu ya kushirikishwa; atakayefanya jambo lolote akamshirikisha pamoja nami mwingine nitamuacha na shirki yake au (na mshirika wake).
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msizifanye nyumba zenu kuwa makaburi, na wala msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, na mniombee rehema juu yangu, kwani maombi yenu hunifikia mahala popote mtakapokuwa.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakaye shuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika nakuwa Muhammadi ni mjumbe wake na ni mja wake, nakuwa Issa ni mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na neno lake alilolipeleka kwa Mariam na ni roho toka kwake, na pepo ni kweli na moto ni kweli, Atamuingiza Mwenyezi Mungu peponi kulingana na yale aliyokuwa nayo katika matendo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayekutana na Mwenyezi Mungu hali yakuwa hamshirikishi na chochote ataingia peponi, na atakaye kutananaye hali yakuwa anamshirikisha na chochote ataingia motoni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakaye nidhamini kuhifadhi ulimi wake na tupu yake nitamdhamini kuingia peponi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Dhikri bora ni: Laa ilaaha ila LLah
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Pepo iko karibu na mmoja wenu kuliko hata kisigino cha kiatu chake, na moto mfano huo huo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Swala tano, na Ijumaa mpaka Ijumaa, na ramadhani mpaka ramadhani vinafuta madhambi yaliyo kati yake, yatakapoepukwa madhambi makubwa.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haumpati muislamu uchovu wala maradhi, wala msongo, wala huzuni, wala udhia, wala shida, hata mwiba unaomchoma, ispokuwa anamfutia Mwenyezi Mungu kupitia hilo makosa yake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Umezingirwa moto kwa mambo yenye kutamanisha, na imezingirwa pepo kwa yenye kuchukiza.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haki za Muislamu juu ya muislamu ni tano: Kujibu salamu, na kumtembelea mgonjwa, na kusindikiza jeneza, na kuitika wito, na kumtakia rehma mwenye kupiga chafya.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amrehemu Mwenyezi Mungu mja mpole anapouza, na anaponunua, na anapodai
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa mtu mmoja akiwadai watu, na alikuwa akimwambia kijana wake: Ukimuendea mwenye hali ngumu msamehe, huenda Mwenyezi Mungu akatusamehe na sisi, akakutana na Mwenyezi Mungu akamsamehe.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakayetoka katika kutafuta elimu basi huyo yuko katika njia ya Mwenyezi Mungu mpaka atakaporejea.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Watakapo kutana waislamu wawili kwa mapanga yao basi muuwaji na muuliwaji wote motoni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika halali iko wazi na hakika haramu iko wazi, na kati ya hayo kuna mambo yenye kutatiza hawayafahamu wengi katika watu, atakaye yaepuka mambo yenye kutatiza basi atakuwa ameitakasa dini yake na heshima yake, na atakayetumbukia katika mambo yenye kutatiza atakuwa katumbukia katika haramu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu hatazami katika mili yenu wala katika sura zenu, lakini anaangalia katika nyoyo zenu na matendo yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika matendo yote huzingatiwa nia, na hakika kila mtu hulipwa kwa lile alilolinuia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kwamba mtu mmoja alimwambia Mtume -Rehma na amani ziwe juu yake- Niusie, Akasema: Usikasirike, akarudiarudia swali na Mtume naye akaendelea kumwambia: Usikasirike.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Laiti nyinyi mgetegemea kwa Mwenyezi Mungu ukweli wa kumtegemea, basi angekuruzukuni kama anavyowaruzuku ndege, wanatoka asubuhi wakiwa na njaa, wanarudi jioni wakiwa wameshiba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ametenda dhambi mja, akasema: Ewe Mola wangu nisamehe mimi dhambi langu, akasema Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka: Mja wangu katenda dhambi, na akajua kuwa ana Mola anayesamehe dhambi, na analichukua dhambi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika waadilifu mbele ya Mwenyezi Mungu watakuwa katika majukwaa ya nuru: wale wanaofanya uadilifu katika hukumu zao, na watu wao na yale waliyoyatawala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Je mnajua ni nini kusengenya? wakasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wajuzi, akasema: ni kumsema kwako ndugu yako kwa yale anayoyachukia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika watu wanaovuruga katika mali ya Mwenyezi Mungu bila haki, watakuwa na adhabu ya moto siku ya kiyama.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Jiepusheni na dhana, kwani dhana ni maneno ya uongo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kila mwanadamu ni mkosefu, na mbora wa wakosefu ni wale wenye kutubia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kila wema ni sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Usidharau kabisa katika wema kitu chochote, hata kama nikukutana na ndugu yako kwa uso mkunjufu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hawi mtu mkali kwa miereka, hakika mkali ni yule anayemiliki nafsi yake wakati wa hasira
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayejulisha juu ya kheri yoyote, atapata malipo mfano wa malipo ya mfanyaji wake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msiwatukane wafu: kwani wao tayari wameyaendea yale waliyoyatanguliza
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Si halali kwa muislamu kumhama ndugu yake zaidi ya siku tatu, wanakutana: huyu anampuuza huyu, na huyu anampuuza huyu, na mbora wao ni yule anayeanza kwa salamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haingii peponi mkataji (udugu)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haingii peponi mfitinishaji
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayependa kukunjuliwa katika riziki yake, na kucheleweshwa katika ajali yake basi naaunge udugu wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mahala alipo karibu zaidi mja na Mola wake ni pale anapokuwa kasujudu, zidisheni dua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na aseme la kheri au anyamaze, Na Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu jirani yake, Na Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu mgeni wake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asiyewahurumia watu hatomuhurumia Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Watu wanaochukiza zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni mgomvi zaidi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Maneno yanayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni manne, haikudhuru kwa lolote utakaloanza nalo: Sub-haanallah (Ametakasika Mwenyezi Mungu) Al-hamdulillaah (Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu), Na, Laa ilaaha illa llaah, (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu), Na Allahu Akbar (Mwenyezi Mungu Mkubwa)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Vinavyowaingiza watu kwa wingi peponi ni uchamungu na tabia njema.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haya (Aibu) ni katika imani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika dua ndiyo ibada
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Maneno mawili yanapendeka sana kwa Ar-Rahmani (Mwingi wa Rehema) ni mepesi sana katika ulimi, ni mazito sana katika mizani: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema zake, Sub-haana llaahil A'dhwiim- Ametakasika Mwenyezi Mungu Mtukufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna kitu kitukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko dua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayerudisha heshima ya ndugu yake, basi Mwenyezi Mungu atauweka mbali uso wake na moto siku ya kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayesema: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema ni zake- kwa siku mara mia moja, atasamehewa makosa yake hata kama yatakuwa mfano wa povu la bahari
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayesema: Laa ilaaha illa llaahu wahdahu Laa shariika lahu, Lahul Mulku walahul Hamdu, Wahuwa a'laa kulli shay in Qadiir (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, yeye pekee asiye na mshirika, Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, Naye juu ya kila kitu ni muweza), akasema hivyo mara kumi, Atakuwa sawa na aliyeacha huru nafsi nne katika watoto wa Ismail.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenye kumtakia Mwenyezi Mungu kheri kwake humpa ufahamu katika dini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu anampenda mja mchamungu mwenye kutosheka mwenye kujificha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hakatai marashi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mkamilifu zaidi wa waumini katika imani ni yule mwenye tabia nzuri zaidi kati yao, na mbora wenu ni mbora wenu kwa wake zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika upole hauwi katika kitu ispokuwa utakipendezesha, na wala hauondolewi katika kitu ispokuwa utakiharibu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu huridhika kwa mja anapokula chochote, akamshukuru juu ya hicho, au akanywa chochote akamshukuru juu ya hicho.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika muumini hufikia kwa tabia yake njema nafasi ya mfungaji mwenye kusimama usiku.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika katika wabora wenu ni wale wenye tabia njema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu humpa muda mtu dhalimu, basi anapomshika hamuachii.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Sijaacha baada yangu fitina ambayo inamadhara zaidi kwa wanaume kuliko wanawake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Fanyeni wepesi na wala msifanye uzito, na toeni habari njema na wala msiwakimbize watu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayeshuka mahala popote kisha akasema: -A'udhu bikalimaati llaahit taammaati min sharri maa khalaqa- (Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyotimia, kutokana na shari ya vile alivyoviumba), hakitomdhuru chochote mpaka aondoke mahala pake hapo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hawezi kuamini mmoja wenu mpaka niwe napendeka kwake zaidi kuliko mtoto wake, na mzazi wake, na watu wote.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kusema kwangu Sub-haana llaah, wal hamdulillaah, wa laa ilaaha illa llaahu wallaahu Akbaru,- Ametakasika Mwenyezi Mungu na kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu na hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu Mkubwa.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayezisoma aya mbili za mwisho wa suratul Baqara katika wakati wa usiku zitamtosheleza
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayesoma herufi moja katika kitabu cha Mwenyezi Mungu basi atapata jema moja na jema hilo kwa mema kumi mfano wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenye kukitegemea kitu hufungamanishwa kwacho
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Wenye huruma huwahurumia Ar-Rahmani -Mwingi wa huruma-, wahurumieni watu wa ardhini atakuhurumieni aliyeko mbinguni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amekataza Mtume wa Allah -Rehma na amani ziwe juu yake kunyoa panki(Kiduku)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Tumekatazwa kujilazimisha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna mja yeyote atakayeshuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammdi ni mja wake kwa kusadikisha kutoka moyoni mwake ispokuwa atamharamisha Mwenyezi Mungu kuingia motoni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe kijana, mtaje Mwenyezi Mungu, na ule kwa mkono wako wa kulia, na ule chakula kilicho mbele yako" kinachokuelekea"
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapo kula mmoja wenu basi na ale kwa mkono wake wa kulia, na atakapo kunywa basi na anywe kwa mkono wake wa kulia, kwani shetani anakula kwa mkono wako wake wa kushoto, na anakunywa kwa mkono wake wa kushoto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Twahara (usafi) ni sehemu ya imani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Basi tambua kuwa haki za Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni wamuabudu yeye na wala wasimshirikishe na kitu chochote, na haki za waja kwa Mwenyezi Mungu asimwaadhibu yeyote ambaye hajamshirikisha yeye na chochote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakaye kufa hali ya kuwa hamshirikishi Mwenyezi Mungu na kitu chochote ataingia peponi, na atakaye kufa akiwa anamshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu chochote ataingia motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nieleze ndani ya Uislamu kauli ambayo sitomuuliza yeyote zaidi yako, akasema: "Sema: Nimemuamini Mwenyezi Mungu, kisha kuwa na msimamo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kwa hakika Mwenyezi Mungu atamchagua mtu mmoja katika umma wangu mbele ya mkusanyiko wa watu siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenyezi Mungu alipoumba Pepo na Moto alimtuma Malaika Jibril -Amani iwe juu yake- aende peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Shikamaneni na kumcha Mwenyezi Mungu, na usikivu na utii, hata kama (mzungumzaji) atakuwa mtumwa tena muhabeshi (Muethiopia), na mtakuja kuona baada yangu hitilafu nyingi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapo sema Muadhini: Allahu Akbaru Allahu Akbaru, kisha akasema mmoja wenu: Allahu Akbaru Allahu Akbaru
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Nimeigawa swala baina yangu na mja wangu nusu mbili, na mja wangu ana haki ya kupata alichooomba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msivae hariri nyepesi wala nguo zilizofumwa kwa hariri, na wala msinywe katika vyombo vya dhahabu wala fedha, na wala msile katika sahani zake, kwani hivyo ni vyao duniani na ni vyenu Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msivae hariri; kwani atakayeivaa duniani hatoivaa Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alitoka Muawiya- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- akakuta duara msikitini, akasema: Nini kimewakalisheni? wakasema: tumekaa tunamtaja Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alipita Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika makaburi mawili, Akasema: Hakika hawa wawili wanaadhibiwa, na hawadhibiwi kwa madhambi makubwa; ama mmoja wao: alikuwa hajisitiri kutokana na mkojo, na ama huyu mwingine: Alikuwa akitembea akiwafitinisha watu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika safari, nikanyoosha mikono ili nimvue viatu vyake (khufu), akasema; ziache; kwani hakika mimi nimezivaa zikiwa safi, akafuta juu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Je anaweza kulala mmoja wetu akiwa na janaba? Akasema: Ndiyo, atakapotawadha mmoja wenu basi na alale
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapotawadha mmoja wenu basi na aweke puani mwake maji, kisha apenge, na atakayestanji kwa mawe basi ayafanye kuwa witiri, na atakapoamka mmoja wenu toka usingizini mwake basi na aoshe mikono yake kabla hajaiingiza katika chombo mara tatu, kwani hakika mmoja wenu hajui ni wapi ulilala mkono wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapoingia mtu nyumbani kwake, akamtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa kuingia kwake na wakati wa kula kwake husema shetani kuwaambia jamaa zake: Hamna malazi wala chakula cha usiku kwenu, na atakapoingia akawa hakumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa kuingia kwake, shetani husema: mmepata malazi na chakula cha usiku
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mchungeni(mfuatilieni) Muhammadi -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa watu wa nyumba yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika dunia ni tamu, ni ya kijani, na hakika Mwenyezi Mungu anakumilikisheni ndani yake aone ni namna gani mtafanya, iogopeni dunia na waogopeni wanawake; kwani hakika fitina ya kwanza ya wana wa Israeli ilikuwa kwa wanawake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
"Haya (Aibu) haiji ila kwa kheri"
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asishike mmoja wenu utupu wake kwa mkono wake wa kulia akiwa anakidhi haja ndogo, na asijifute haja ndogo au kubwa kwa mkono wake wa kulia na asipumulie ndani ya chombo anachonywea.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Wewe pamoja na uliyempenda
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika bila shaka mfano wa rafiki mwema na rafiki muovu, ni kama mfano wa mbeba miski, na mfua vyuma
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe mwenye kuzigeuza nyoyo uthibitishe moyo wangu katika Dini yako.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayemuomba Mwenyezi Mungu shahada (yaani kufa shahidi) kwa ukweli, basi atamfikisha daraja ya mashahidi hata kama atafia juu ya godoro lake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Halitoacha kumfika balaa muumini wa kiume na muumini wa kike katika nafsi yake na watoto wake na mali yake mpaka akutane na Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwa hana dhambi lolote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hana mja wangu muumini toka kwangu malipo yoyote pindi ninapomchukua kipenzi chake katika familia yake duniani kisha akasubiri (malipo mazuri) zaidi ya pepo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msiziombee mabaya nafsi zenu,wala msiwaombee vibaya watoto wenu,wala msiziombee vibaya mali zenu,nakhofia dua hizo zisikutane na muda ambao haombwi Mwenyezi Mungu katika muda huo chochote isipokuwa anakujibuni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hujibiwa mmoja wenu anapokuwa hajafanya haraka: anasema: Nimemuomba Mola wangu, na wala sijaona ananijibu mimi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ni dua ipi inasikilizwa zaidi? Akasema: katikati ya mwisho wa usiku, na mwisho wa swala za faradhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hebu rudi kwa wazazi wako, na ukaishi nao vizuri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Dinari bora anayoitoa mtu: ni Dinari anayoitoa kwa familia yake, na Dinari anayoitoa kwa mnyama wake katika njia ya Mwenyezi Mungu, na Dinari anayoitoa kwa jamaa zake katika njia ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapoona mmoja wenu ndoto anayoipenda, basi hiyo imetoka kwa Mwenyezi Mungu, na amshukuru Mwenyezi Mungu juu yake, na aisimulie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ajabu iliyoje ya jambo la muumini, hakika jambo lake lote ni kheri, na hakuna hilo kwa yeyote ila kwa muumini: akipatwa na jambo lenye kufurahisha anashukuru ikawa hilo ni kheri kwake, na akipatwa na madhara anasubiri likawa hilo ni kheri kwake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapopiga chafya anaweka mkono wake au nguo yake juu ya kinywa chake, na anapunguza sauti yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Je nisikuelezeni kwa kile ambacho ninakiogopea zaidi kwenu nyinyi kuliko hata masihi dajali? Wakasema: Tueleze ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, akasema: Ni shirki iliyofichikana, anasimama mtu kuswali anapendezesha swala yake kwakuwa anaona kuna mtu anamtazama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ee fulani, una nini wewe? kwani hukuwa unaamrisha mema na unakataza mabaya? atasema: Ndivyo, nilikuwa nikiamrisha mema na wala siyafanyi, na ninakataza mabaya na ninayafanya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, wala nyumba zenu kuwa makaburi, na nitakieni rehma, kwani dua zenu hunifikia popote mlipo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtakapo vaa, na mtakapo tawadha, basi anzeni na kuliani kwenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayewalea mabinti wawili mpaka wakafikia utu uzima atakuja siku ya kiyama mimi na yeye ni kama vidole hivi viwili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, Hamtoingia peponi mpaka muamini, na hamtoamini mpaka mpendane, je nisikufahamisheni juu ya jambo ambalo mkilifanya mtapendana? toleaneni salamu kwa wingi kati yenu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ni amali ipi inayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu? Akasema: Ni (kuiswali) swala kwa wakati wake. Nikasema: kisha nini? Akasema: Ni kuwatendea wema wazazi wawili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hili ni jiwe lililotupwa motoni tangu miaka sabini, anaporomoka motoni sasa hivi mpaka kaishia katika kina chake ndio maana mkasikia kishindo chake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba mtu mmoja alikula kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa mkono wake wa kushoto, akasema: kula kwa mkono wako wa kulia, akasema: siwezi. akasema: Hutoweza, hakuna kilichomzuia isipokuwa ni kiburi, basi hakuweza tena kuunyanyua kufika kinywani kwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mikosi ya ndege ni shirki, na hakuna yeyote miongoni mwetu ispokuwa (ana chembe ya hilo), lakini Mwenyezi Mungu huliondoa kwa kumtegemea
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa kwa Saidi bin Jubair akasema: Ni nani kati yenu aliyeiona nyota iliyodondoka jana usiku? Nikasema: Mimi, kisha nikasema: Ama mimi sikuwa katika swala, lakini niling'atwa (na Nge)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna kuambukizana maradhi wala kutuhumu mikosi kwa sababu ya ndege, wala mkosi wa Bundi,na aina zingine za ndege,wala kutuhumu kuwa mwezi wa safari unamikosi, au maradhi ya tumbo yanayompata ngamia.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nitampa bendera kesho mtu ambaye anampenda Allah na Mtume wake,na anapendwa na Allah na Mtume wake,kupitia yeye Allah ataleta ushindi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ni nani anayejiapiza kwangu kuwa sitomsamehe fulani? Hakika mimi nimemsamehe,na nimeyaporomosha matendo yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haitokei kuuliwa nafsi yoyote kwa dhulma isipokuwa hupata binadamu wa mwanzo fungu (la dhambi) kutoka katika damu hiyo, kwasababu yeye ndiye muanzilishi wa kwanza kuua.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hivi hukujua kuwa uislamu hufuta madhambi yaliyokuwa kabla yake, na kuwa kuhama kunafuta madhambi yaliyokuwa kabla yake, nakuwa Hija inafuta madhambi yaliyokuwa kabla yake?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mja anaweza kuzungumza neno asilijali ndani yake akateleza kwa neno hilo nakuingia katika moto ambao umbali wake ni baina ya mashariki na magharibi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayesema: -Yaani: anapotoka nyumbani kwake-: Bismillaahi tawakkaltu a'la llaahi -kwa jina la Mwenyezi Mungu nimemtegemea Mwenyezi Mungu, Laa haulaa walaa quwwata illaa billaa- hakuna ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, huambiwa: Umeongozwa na umetoshelezwa na umekingwa, na shetani hujitenga mbali naye
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mcheni Mwenyezi Mungu na mswali swala zenu tano, na mfunge mwezi wenu, na mtekeleze zaka za mali zenu, na muwatii viongozi wenu, mtaingia pepo ya Mola wenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapokutana mmoja wenu na ndugu yake basi na amsalimie, ukiwatenganisha kati yao mti, au ukuta, au jiwe, kisha akakutana naye tena basi amsalimie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Je! nikujulisheni mambo ambayo yakifanyika Allah hufuta madhambi na hupandisha daraja kwa mambo hayo? wakasema: ndiyo, Ewe Mtume wa Allah, akasema: Kutawadha vizuri wakati wa baridi, na kuzidisha hatua kwenda msikitini, na kusubiria swala baada ya swala huko ndiko kuizuia nafsi katika mambo ya kheri.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Je nikujulisheni matendo yenu bora, na matukufu mbele ya mfalme wenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mimi ninajua neno ambalo laiti angelisema yangemuondokea yaliyompata, lau angelisema: Au'dhubillaahi minshaitwanir-rajiim, -Najilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa, yangemuondokea yaliyompata
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ndoto nzuri hutoka kwa Mwenyezi Mungu, na njozi hutoka kwa shetani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Zuia ulimi wako, na ikutosheleze nyumba yako, na ulie juu ya makosa yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika peponi kuna daraja mia moja kaziandaa Mwenyezi Mungu kwaajili ya wenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu kati ya daraja mbili ni kama masafa ya baina ya mbingu na ardhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amesema Mwenyezi Mungu -Mtukufu- mimi niko katika dhana ya mja wangu kwangu, na mimi niko pamoja naye pindi anaponikumbuka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayependezwa na kumtazama mtu miongoni mwa watu wa peponi basi na amtazame huyu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Laiti Dunia ingelingana na ubawa wa mbu kwa thamani yake mbele ya Allah mtukufu basi kafiri asingekunywa fundo moja la maji.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), atakayewapata wazazi wake wawili wakati wa ukubwa mmoja wao au wote wawili na akawa hakuingia peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Wametangulia watu wa kipekee
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Anafunga shetani juu ya kisogo cha kichwa cha mmoja wenu, pindi anapolala, mafundo matatu, anapiga katika kila fundo: Unatakiwa kulala usiku mrefu basi lala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Macho ya aina mbili hautoyagusa moto: Jicho lililolia kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu, na jicho lililokesha likilinda kwaajili ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika kila umma una mtihani wake, na mtihani wa umma wangu: ni mali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Umma wangu wote watasalimika isipokuwa wenye kuyatangaza (madhambi)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hato msitiri mja mja mwenzie duniani isipokuwa atamsitiri Mwenyezi Mungu siku ya kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asife mmoja wenu isipokuwa naye awe na dhana nzuri na Mwenyezi Mungu Mtukufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikutana na Ibrahimu usiku niliochukuliwa, Akasema: Ewe Muhammadi wafikishie umma wako salamu zangu, na uwaeleze kuwa pepo ina udongo mzuri, ina maji matam, nakuwa imenyooka na kulingana sawa, nakuwa mimea yake: ni (kusema) Sub-haana llaah -Ametakasika Mwenyezi Mungu, Na Alhamdulillaah -Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu, Na Laa ilaaha illa llaah -Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Allaahu Akbar -Mwenyezi Mungu Mkubwa.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haijabakia katika utume isipokuwa viashiria vya habari njema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Lau kama ningekuwa na dhahabu kubwa mfano wa mlima Uhudi, basi ningependa zisipite siku tatu nikiwa namiliki chochote katika mali hiyo zaidi ya kile ninachokihifadhi kwaajili ya kulipa madeni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ikiwa kama utakuwa kama ulivyosema, basi ni kana kwamba unawalisha majivu ya moto (dhambi wanazozipata ni kama mtu anayekula majivu ya moto), Na bado anaendelea kuwa pamoja nawe msaidizi kutoka kwa Mwenyezi Mungu dhidi yao, madam bado uko katika hali hiyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Si chochote dunia katika Akhera isipokuwa ni kama mfano wa mmoja wenu anapoweka kidole chake baharini, kisha atazame kimerudi na nini?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna watu wowote watasimama katika kikao ambacho hawamtaji Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake, isipokuwa watanyanyuka mithili ya mzoga wa punda, na wanakua na majuto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hainifurahishi mimi kumiliki dhahabu mfano wa mlima huu wa Uhudi, zikapita siku tatu nikawa hata na dinari moja (katika mali hiyo) isipokuwa kiasi ninachokihifadhi kwaajili ya kulipa deni, isipokuwa niseme kwa waja wa Mwenyezi Mungu hivi na vile.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mfano wa yule anayemtaja Mola wake na yule asiyemtaja Mola wake ni mfano wa aliyehai na aliyekufa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika katika yale ninayoyahofia zaidi kwenu nyinyi baada yangu ni yale yatakayofunguliwa kwenu miongoni mwa ua la dunia na pambo lake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni nani mwenye haki zaidi ya kumfanyia wema wa karibu? akasema: mama yako, kisha mama yako kisha mama yako, kisha baba yako, kisha anayefuata kwa ukaribu kisha nayemfuata kwa ukaribu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayetoa vitu vya namna mbili katika njia ya Mwenyezi Mungu huitwa katika milango ya pepo, ewe mja wa Mwenyezi Mungu hii ni kheri, atakayekuwa miongoni mwa watu wa swala ataitwa katika mlango wa swala, atakayekuwa katika watu wa jihadi ataitwa katika mlango wa jihadi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayeniona mimi ndotoni basi ataniona akiwa macho -au ni kana kwamba kaniona akiwa macho- hajifananishi shetani na mimi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mwenye adhabu nyepesi zaidi katika watu wa motoni siku ya kiyama, ni mtu atawekewa ndani ya nyayo zake makaa mawili ya moto, utakuwa ukitokota kupitia hayo ubongo wake, na yeye atakuwa akiona kuwa hakuna mtu mwenye adhabu kali zaidi yake, na hakika kumbe yeye ndiye mwenye adhabu nyepesi kuliko wao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yanamfuata maiti mambo matatu: familia yake na mali yake na matendo yake, vinarudi vitu viwili na kinabakia kimoja: wanarudi familia yake na mali yake, na yanabakia matendo yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amsalimie aliyepanda anayetembea, na anayetembea aliyekaa, na wachache kwa wengi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna kitu chenye uzito zaidi katika mizani ya muumini siku ya Kiyama kuliko tabia njema, na hakika Mwenyezi Mungu anamchukia mtu muovu mwenye kauli chafu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mtume rehema na amani ziwe juu yake alitoka kwetu sisi, tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tumekwishafahamu ni vipi tutakusalimu, sasa ni vipi tutakutakia Rehema?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Muumini mwenye nguvu ni bora na anapendeka kwa Mwenyezi Mungu kuliko muumini dhaifu, na katika kila kheri,
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ilikuwa Dua aiombayo zaidi Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-:ni "Ewe Mola wetu Mlezi, tupe duniani mazuri, na Akhera mazuri, na utukinge na adhabu ya moto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Bwana wa Istighfari (Dua ya kuomba msamaha)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ogopeni dhulma, kwa hakika dhulma ni giza siku ya kiyama. Na ogopeni tamaa, kwa hakika tamaa iliwaangamiza walio kuwepo kabla yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ni, ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Sema Yeye ni Mwenyezi Mungu mmoja tu" na sura mbili za kinga unapofika nyakati za jioni na nyakati za asubuhi mara tatu, zitakutosheleza kila kitu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Sema: Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiyekuwa na mshirika, Mwenyezi Mungu mkubwa mno, na kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu kwa wingi, na ametakasika Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu, na hapana ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu mwenye nguvu na hekima
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Adh-kari za baada ya sala ya faradhi hapati hasara msomaji au mfanyaji wake, kusema Sub-haana llahi mara thelathini na tatu (33), Al-hamdulillahi mara thelethini na tatu (33), Allahu Akbaru mara thelathini na nne (34)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Aina mbili za watu ni miongoni mwa watu wa motoni, sijawaona (katika zama zake Mtume), watu walio na mijeledi mithili ya mikia ya Ng'ombe wakiwapiga watu, na wanawake waliovaa na wako uchi, wanenguaji wakatikaji
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asiangalie mwanaume katika uchi wa mwanaume mwenzie, wala mwanamke kutazama uchi wa mwanamke mwenzie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Muislamu wa kweli ni yule wanayepata Amani waislamu wenzake kutokana na ulimi wake na mkono wake, na mhamaji ni yule mwenye kuyahama yale aliyoyakataza Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi sijaacha dhambi yoyote wala maasi yoyote isipokuwa nimeyafanya, akasema: "Hivi wewe hautamki neno la shahada "Ash-hadu an-laa ilaaha illa llahu wa anna Muhamadan rasuulullah?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Shetani humjia mmoja wenu na akamwambia: Ni nani aliumba kitu fulani? Mpaka anafikia kusema ni nani alimuumba Mola wako? Basi ikiwa atafikia kuuliza hivyo basi na ajikinge kwa Mwenyezi Mungu na awache kuuliza maswali hayo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Matendo yapo ya aina sita na watu wapo wako aina nne, basi kuna watu wa aina mbili wanaostahiki malipo, na malipo yao huwa sawa na matendo yao, na jema moja hulipwa kwa kumi mfano wake, na jema moja huzidishwa mpaka kufikia mema mia saba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kwa hakika miongoni mwa alama za Kiyama ni kuondolewa elimu, na kuzidi ujinga, na kukithiri uzinifu, unywaji pombe, na wanaume watakuwa wachache na wanawake watakuwa wengi mpaka itafikia wanawake hamsini kusimamiwa na mwanaume mmoja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakitosimama Kiyama mpaka apite mtu juu ya kaburi la mtu aseme: Natamani ningekua nafasi yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mauti yataletwa yakiwa kama dume la Kondoo mwenye rangi mchanganyiko ya weusi na weupe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Moto wenu wa Dunia ni sawa na sehemu tu ya sabini itokanayo na moto wa Jahannam
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakayenisingizia mimi uongo kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake kuwa ni motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alitaja jambo fulani, akasema: "Jambo lenye kuogopesha litakuwa wakati itakapo ondoka elimu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msijifunze elimu kwa ajili ya kujifaharisha kuwa ni katika maulama, wala kwa kujadiliana na wasiokuwa na elimu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amepigia mfano Mwenyezi Mungu wa njia iliyonyooka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Je anapenda mmoja wenu pindi atakaporudi kwa mke wake apate Ngamia watatu wenye mimba na walio nenepa?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ataambiwa msomaji wa Qur'ani: Soma na upande daraja, na soma kwa utulivu kama ulivyokuwa ukisoma Duniani, kwa hakika upandaji wa cheo chako utakomea katika Aya ya mwisho utakayoisoma
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenye kuisoma Qur'ani kwa sauti ya wazi ni kama mwenye kutoa sadaka hadharani, na mwenye kuisoma Qur'ani kwa siri ni kama mwenye kuficha sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
walikuwa wakitusomea Aya kumi kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, hivyo hawakuwa wakichukua Aya kumi zingine mpaka wawe wamekwishayafanyia kazi yaliyo ndani ya aya hizo kumi kwa kujifunza na kuyafanyia kazi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe baba Mundhir, hivi unaijua aya gani katika kitabu cha Mwenyezi Mungu ambayo ni tukufu zaidi?" Akasema: Nikasema: {Allahu laa ilaaha illa huwal hayyul qayyuum} Al-baqara: Basi akanipiga katika kifua changu, akasema: Nakuombea Mwenyezi Mungu elimu ikupe furaha ewe baba Mundhir
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapolala kitandani kwake wakati wa kila usiku alikuwa akikusanya viganja vyake, kisha akivipuliza na kuvisomea : {Qul-huwallahu Ahad}, na {Qul-A uudhu birabbil falaq} na (Qul-Auudhu birabbi naas }
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ikiwa utawaona wenye kufuata Aya zenye kutatiza basi hao ndiyo ambao Mwenyezi Mungu amewataja katika aya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna mtu yeyote atakayetenda dhambi, kisha akasimama akajitwaharisha, kisha akaswali, kisha akamuomba Allah msamaha, isipokuwa Mwenyezi Mungu humsamehe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Akasema: "Watahesabiwa kwa hiyana waliyokufanyia na kukuasi na kukudanganya, na itahesabiwa adhabu yako uliyowapa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Sema: Laa ilaaha illa llahu, nitakutolea ushuhuda wa kusilimu kwa maneno hayo siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kisha hakika bila shaka mtakuja kuulizwa kuhusu neema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtakapo msikia muadhini basi semeni mfano wa yale anayo yasema, kisha mnitakie rehema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi aseme: Allaahummaf-tah lii abwaaba rahmatika (Ewe Mola wangu, nifungulie milango ya rehema zako), na akitoka aseme: Allaahumma innii as-aluka min fadhlika (Ewe Mola wangu ninakuomba unipe katika fadhila zako)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Huyo ni Shetani anaitwa Khinzab, ukimuhisi basi haraka sana taka ulinzi kutoka kwa Allah dhidi yake, na uteme kushotoni kwako mara tatu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa