Orodha ya Hadithi

Hivi nisikuelezeni juu ya dhambi kubwa kuliko yote?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapo mpenda mtu ndugu yake amwambie kuwa anampenda.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
"Jiepusheni na mambo saba yenye kuangamiza, wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni yapi hayo? Akasema: Ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu, na uchawi, na kuuwa nafsi aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu ispokuwa kwa haki, na kula riba, na kula mali ya yatima, na kukimbia siku ya mapambano, na kuwazulia machafu wanawake waumini wenye kujihifadhi wenye kujizuia na machafu".
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amrehemu Mwenyezi Mungu mja mpole anapouza, na anaponunua, na anapodai
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa mtu mmoja akiwadai watu, na alikuwa akimwambia kijana wake: Ukimuendea mwenye hali ngumu msamehe, huenda Mwenyezi Mungu akatusamehe na sisi, akakutana na Mwenyezi Mungu akamsamehe.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kwamba mtu mmoja alimwambia Mtume -Rehma na amani ziwe juu yake- Niusie, Akasema: Usikasirike, akarudiarudia swali na Mtume naye akaendelea kumwambia: Usikasirike.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika waadilifu mbele ya Mwenyezi Mungu watakuwa katika majukwaa ya nuru: wale wanaofanya uadilifu katika hukumu zao, na watu wao na yale waliyoyatawala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Jiepusheni na dhana, kwani dhana ni maneno ya uongo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Usidharau kabisa katika wema kitu chochote, hata kama nikukutana na ndugu yako kwa uso mkunjufu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hawi mtu mkali kwa miereka, hakika mkali ni yule anayemiliki nafsi yake wakati wa hasira
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayejulisha juu ya kheri yoyote, atapata malipo mfano wa malipo ya mfanyaji wake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haingii peponi mfitinishaji
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na aseme la kheri au anyamaze, Na Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu jirani yake, Na Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu mgeni wake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asiyewahurumia watu hatomuhurumia Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Watu wanaochukiza zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni mgomvi zaidi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Vinavyowaingiza watu kwa wingi peponi ni uchamungu na tabia njema.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haya (Aibu) ni katika imani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayerudisha heshima ya ndugu yake, basi Mwenyezi Mungu atauweka mbali uso wake na moto siku ya kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu anampenda mja mchamungu mwenye kutosheka mwenye kujificha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mkamilifu zaidi wa waumini katika imani ni yule mwenye tabia nzuri zaidi kati yao, na mbora wenu ni mbora wenu kwa wake zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika upole hauwi katika kitu ispokuwa utakipendezesha, na wala hauondolewi katika kitu ispokuwa utakiharibu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika muumini hufikia kwa tabia yake njema nafasi ya mfungaji mwenye kusimama usiku.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika katika wabora wenu ni wale wenye tabia njema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu humpa muda mtu dhalimu, basi anapomshika hamuachii.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Fanyeni wepesi na wala msifanye uzito, na toeni habari njema na wala msiwakimbize watu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Wenye huruma huwahurumia Ar-Rahmani -Mwingi wa huruma-, wahurumieni watu wa ardhini atakuhurumieni aliyeko mbinguni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amekataza Mtume wa Allah -Rehma na amani ziwe juu yake kunyoa panki(Kiduku)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Tumekatazwa kujilazimisha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alipita Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika makaburi mawili, Akasema: Hakika hawa wawili wanaadhibiwa, na hawadhibiwi kwa madhambi makubwa; ama mmoja wao: alikuwa hajisitiri kutokana na mkojo, na ama huyu mwingine: Alikuwa akitembea akiwafitinisha watu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mimi ninajua neno ambalo laiti angelisema yangemuondokea yaliyompata, lau angelisema: Au'dhubillaahi minshaitwanir-rajiim, -Najilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa, yangemuondokea yaliyompata
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hato msitiri mja mja mwenzie duniani isipokuwa atamsitiri Mwenyezi Mungu siku ya kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna kitu chenye uzito zaidi katika mizani ya muumini siku ya Kiyama kuliko tabia njema, na hakika Mwenyezi Mungu anamchukia mtu muovu mwenye kauli chafu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ogopeni dhulma, kwa hakika dhulma ni giza siku ya kiyama. Na ogopeni tamaa, kwa hakika tamaa iliwaangamiza walio kuwepo kabla yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asiangalie mwanaume katika uchi wa mwanaume mwenzie, wala mwanamke kutazama uchi wa mwanamke mwenzie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Muislamu wa kweli ni yule wanayepata Amani waislamu wenzake kutokana na ulimi wake na mkono wake, na mhamaji ni yule mwenye kuyahama yale aliyoyakataza Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakayenisingizia mimi uongo kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake kuwa ni motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa