عن عبد الله بن عمرو بن العاص - رضي الله عنهما- قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «إن المُقْسِطين عند الله على منابر من نور: الذين يعدلون في حكمهم وأهليهم وما ولَوُاْ».
[صحيح] - [رواه مسلم. ملحوظة: في صحيح مسلم زيادة على ما في رياض الصالحين: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: «إن المقسطين عند الله على منابر من نور، عن يمين الرحمن -عز وجل-، وكلتا يديه يمين»]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillah bin Amri bin Aaswi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Hakika waadilifu mbele ya Mwenyezi Mungu watakuwa katika majukwaa ya nuru: wale wanaofanya uadilifu katika hukumu zao, na watu wao na yale waliyoyatawala".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Katika hadithi kuna habari njema kwa wale wanaohukumu kwa uadilifu baina ya watu ambao wako chini ya mamlaka yao na hukumu yao, nakuwa wao watakuwa juu ya majukwaa ya nuru ya uhakika kama takrima kwao siku ya kiyama mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa uadilifu na kuhimizwa juu yake.
  2. Kubainishwa daraja ya waadilifu siku ya kiyama.
  3. Kutofautiana kwa daraja za watu wenye imani siku ya kiyama kila mmoja kulingana na matendo yake.
  4. Mfumo wa kutia hamasa ni katika mifumo ya ufikishaji ambao unamuhasisha mfikishiwaji katika utiifu.
  5. Kuthibitishwa mkono na -upande wa- kulia kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu bila kupindisha au kuulizauliza au kufananisha au kupotosha.