عن شداد بن أوس رضي الله عنه مرفوعًا:« إن الله كتب الإحسانَ على كل شيء، فإذا قتلتم فأحسِنوا القِتلةَ وإذا ذبحتم فأحسِنوا الذِّبحة، وليحد أحدُكم شَفْرَتَه ولْيُرِحْ ذبيحتَهُ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Shaddad bin Ausi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u "Hakika Mwenyezi Mungu amefaradhisha (kutenda) wema katika kila kitu, hivyo mtakapoua basi uweni vizuri (kwa wema), na mtakapochinja basi chinjeni vizuri, na anowe mmoja wenu makali yake, na akistareheshe kichinjwa chake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Muislamu anatakiwa kuwa mwema katika nia yake na siri yake, na anatakiwa kuwa mwema katika utiifu wake na ibada zake, na anatakiwa kuwa mwema katika matendo yake anayoyafanya, na anatakiwa kuwafanyia wema watu na wanyama; bali hata katika vile visivyokuwa na uhai. Na hakuna shaka kuwa mwenye kumchinja mnyama ni lazima atamuumiza, na ni lazima amchinje kwaajili ya kunufaika naye, hivyo basi makusudio ni malezi yenye huruma na upole katika nafsi ya muumini ili asighafilike na maana hizo hata kama atakuwa anachinja na anauwa kwa haki,nalo ni angalizo kuwa ikiwa wema umetakiwa katika kuuwa na kuchinja basi kutakiwa katika mambo mengine ndio inakuwa na mkazo zaidi, na katika wema ni kunoa kisu na kumstarehesha mnyama.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani Pashto Kiassam Albanian الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Amri ya kufanya wema nayo ni katika kila kitu kulingana na jinsi kilivyo, Wema katika kutekeleza wajibu wa siri na wa wazi: Ni kuutekeleza kwa namna ya kukamilisha wajibu wake, kiwango hiki cha wema hapa ni wajibu, na ama wema katika kukamilisha sunna zake ni sunna. Na wema katika kuacha maharamisho: Ni kuyamaliza na kuyaacha nje yake na ndani yake, na kiwango hiki hapa ni wajibu, na wema katika kuvumilia juu ya makadirio, ni kuvumilia juu yake na kutochukia, wala kuhamaki, na wema unaotakiwa katika kuamiliana na viumbe na kuishi nao: Ni kusimamia yale aliyoyawajibisha Mwenyezi Mungu katika haki zao. Na wema unaotakiwa katika kuwaongoza viumbe: Ni kwa kusimamia majukumu ya uongozi ya kisheria, na wema katika kuuwa wale wanaofaa kuuliwa katika wanyama: Ni kutoa nafsi yake kwa namna ya haraka zaidi na nyepesi na nzuri, bila kuzidisha katika kumuadhibu, kwasababu ni kumuumiza kusikokuwa na haja.
  2. Upole wa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa waja, nikuwa yeye ameandika wema juu ya kila kitu.
  3. Mwenyezi Mungu Mtukufu ana amri na kwake ndiko kuna hukumu, kwa kauli yake: "Hakika Mwenyezi Mungu ameandika wema" Na kuandika kwa Mwenyezi Mungu kuna aina mbili: Kuandikwa kwa makadirio, na kuandikwa kisheria.
  4. Wema unaenea katika kila kitu, kila kitu wema unawezekana ndani yake kwa kauli yake: "Hakika Mwenyezi Mungu ameandika wema juu ya kila kitu".
  5. Uzuri wa mafundisho ya Mtume rehema na Amani ziwe juu yake- Kwa kupiga mifano; kwasababu mifano husogeza maana karibu, katika kauli yake: Mtakapouwa. mtakapochinja.
  6. Ulazima wa kufanya wema katika kuuwa; kwasababu hii ni sifa ya namna (ya kuuwa) na si ya kitendo.
  7. Wema katika kuchinja, kwa kuchinja katika namna ya kisheria.
  8. Kuharamishwa kumuadhibu mnyama kama kumfanya kuwa Taget (chambo) na kumuacha njaa na kumfunga bila ya kula wala kunywa.
  9. Ukamilifu wa sheria hii na kuenea kwake juu ya kila kheri, na miongoni mwake ni kuwahurumia wanyama na kuwafanyia upole.