عن شداد بن أوس رضي الله عنه مرفوعًا:« إن الله كتب الإحسانَ على كل شيء، فإذا قتلتم فأحسِنوا القِتلةَ وإذا ذبحتم فأحسِنوا الذِّبحة، وليحد أحدُكم شَفْرَتَه ولْيُرِحْ ذبيحتَهُ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Shaddad bin Ausi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u "Hakika Mwenyezi Mungu amefaradhisha (kutenda) wema katika kila kitu, hivyo mtakapoua basi uweni vizuri (kwa wema), na mtakapochinja basi chinjeni vizuri, na anowe mmoja wenu makali yake, na akistareheshe kichinjwa chake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Muislamu anatakiwa kuwa mwema katika nia yake na siri yake, na anatakiwa kuwa mwema katika utiifu wake na ibada zake, na anatakiwa kuwa mwema katika matendo yake anayoyafanya, na anatakiwa kuwafanyia wema watu na wanyama; bali hata katika vile visivyokuwa na uhai. Na hakuna shaka kuwa mwenye kumchinja mnyama ni lazima atamuumiza, na ni lazima amchinje kwaajili ya kunufaika naye, hivyo basi makusudio ni malezi yenye huruma na upole katika nafsi ya muumini ili asighafilike na maana hizo hata kama atakuwa anachinja na anauwa kwa haki,nalo ni angalizo kuwa ikiwa wema umetakiwa katika kuuwa na kuchinja basi kutakiwa katika mambo mengine ndio inakuwa na mkazo zaidi, na katika wema ni kunoa kisu na kumstarehesha mnyama.