Orodha ya Hadithi

Mwenye kuhiji na akawa hakusema maneno machafu wala kutenda matendo machafu, anarudi kama alivyo zaliwa na mama yake (akiwa hana dhambi).
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna swala chakula kikiwa tayari, na hakuna swala kwa mwenye kuhisi haja kubwa na ndogo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Utakaposema kumwambia mwenzio: Nyamaza siku ya ijumaa na Imamu ana khutubu, utakuwa umefanya mchezo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mambo ya kimaumbile ni matano: Kutairiwa, na kuondoa nywele za sehemu ya siri, na kupunguza masharubu, na kupunguza kucha, na kukwapua nywele za kwapani.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Punguzeni masharubu na mfuge ndevu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakayetawadha mfano wa udhu wangu huu, kisha akasali rakaa mbili, na asiizungumzishe ndani ya nafsi yake atasamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mola wangu usilifanye kaburi langu kuwa ni sanamu lenye kuabudiwa, zimekuwa kali hasira za Mwenyezi Mungu juu ya watu walioyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa Misikiti.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Swala nzito juu ya wanafiki: ni swala ya ishaa na swala ya Alfajiri, na lau wangejua yaliyomo ndani ya swala hizo, basi wangeziendea hata kwa kutambaa, na nilitamani niamrishe swala ikimiwe, kisha nimuamrishe mtu awaswalishe watu, kisha niondoke wakiwa pamoja nami wanaume wakiwa na vijinga vya moto twende kwa watu ambao hawahudhurii swala nikazichome nyumba zao kwa moto.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haikubali Mwenyezi Mungu swala ya mmoja wenu atakapotengukwa udhu mpaka atawadhe.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mswaki ni kisafisha kinywa na humridhisha Mola.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Swala tano, na Ijumaa mpaka Ijumaa, na ramadhani mpaka ramadhani vinafuta madhambi yaliyo kati yake, yatakapoepukwa madhambi makubwa.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Muunga udugu sio yule mlipizaji,, lakini muunga udugu ni yule ambaye unapovunjwa udugu wake anauunga
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayefunga ramadhani kwa imani na kwa kutaraji malipo, atasamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakaye simama usiku wenye cheo (Lailatul Qadri) kwa imani na kwa kutaraji malipo, atasamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika halali iko wazi na hakika haramu iko wazi, na kati ya hayo kuna mambo yenye kutatiza hawayafahamu wengi katika watu, atakaye yaepuka mambo yenye kutatiza basi atakuwa ameitakasa dini yake na heshima yake, na atakayetumbukia katika mambo yenye kutatiza atakuwa katumbukia katika haramu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakufai kujidhuru wala kumdhuru mwingine.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Niliyokukatazeni basi yaepukeni, na yale niliyokuamrisheni basi yaleteni katika hayo kadiri muwezavyo, na hakika waliangamia wale waliokuwa kabla yenu, kwa kukithiri maswali yao, na kuhitilafiana kwao na Manabii wao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
"Hakuacha Jibril kuendelea kunihusia kuhusu jirani mpaka nikadhania kwamba yeye atamrithisha".
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika makombe na mahirizi na limbwata ni ushirikina.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msiwatukane wafu: kwani wao tayari wameyaendea yale waliyoyatanguliza
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakaye swali swala ya Al-fajiri atakuwa katika mkataba wa Mwenyezi Mungu hivyo asikutafuteni Mwenyezi Mungu katika mkataba wake kwa chochote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haijawahi kupunguza sadaka chochote katika mali, Na hajawahi kumzidishia Mwenyezi Mungu mja kwa usamehevu (wake) ispokuwa utukufu, na hajawahi kunyenyekea yeyote ispokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu alimnyanyua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mkamilifu zaidi wa waumini katika imani ni yule mwenye tabia nzuri zaidi kati yao, na mbora wenu ni mbora wenu kwa wake zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Dunia ni starehe, na starehe yake bora ni mke mwema.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Toa ewe mwanadamu utapewa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika masharti yenye haki zaidi ya kutekelezwa ni yale ambayo mmehalalisha kwayo nyuchi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Anasema: kila mwisho wa swala anapotoa salamu: "Laa ilaaha illa llaahu wahdahu Laa shariika lahu, Lahul Mulku walahul Hamdu wahuwa a'laa kulli shai in qadiir, Laa haulaa walaa quwwata illaa billaah, walaa na'budu illaa iyyaahu, Lahun ni'matu walahul Fadhlu, walahuth thanaaul hasan, Laa ilaaha Illa llaahu Mukhliswiina lahud diina walau karihal kaafiruun" Yaani: Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, yeye pekee asiye na mshirika, Ufalme ni wake na sifa njema ni zake, naye juu ya kila kitu ni muweza, Hakuna ujanja wala nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu, Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, Na hakuna tunayemuabudu ila yeye, ana neema na ana fadhila, na ana sifa njema, Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu tunamtakasia dini hata kama makafiri watachukia.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna siku ambazo matendo mema yanapendeka zaidi ndani yake kwa Mwenyezi Mungu kama masiku haya.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayeacha swala ya Laasiri itakuwa imeporomoka amali yake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayetawadha na akaufanya vizuri udhu, yatatoka madhambi yake mwilini mwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapotoa mtu kwa familia yake tumizi lolote akitaraji malipo basi hilo kwake ni sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amekataza Mtume wa Allah -Rehma na amani ziwe juu yake kunyoa panki(Kiduku)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Jisafisheni vizuri kutokana na mkojo; kwani adhabu nyingi za kaburini zinatokana na hilo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msiswali makaburini, wala msiyakalie makaburi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hao ni watu ambao anapokufa kwao mja mwema, au mtu mwema, wanajenga juu ya kaburi lake msikiti, na wanachora hapo mapicha, hao ni viumbe waovu mbele ya Mwenyezi Mungu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nimeamrishwa nisujudu kwa viungo saba, kwa paji la uso, na akaashiria kwa mkono wake katika pua yake, na mikono miwili na magoti mawili, na ncha za miguu miwili, na wala tusizikunje nguo na nywele
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akisema kati ya sijida mbili: Allaahumma ghfirlii, warhamnii, wa aafinii, wahdinii. warzuqnii (Ewe Mola wangu nisamehe, na unirehemu, na unipe afya, na uniongoze, na uniruzuku)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehma na Amani ziwe juu yake- anapomaliza swala yake anataka msamaha mara tatu, na anasema: Allaahumma antas salaam, waminkas salaam, Tabaarakta yaa dhal-jalaali wal-ikraam (Ewe Mwenyezi Mungu hakika wewe ni Amani, na Amani hutoka kwako, umetakasika Ewe mwenye Utukufu na ukarimu).
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Swali ukiwa umekaa, ikiwa hutoweza basi ukiwa umekaa, ikiwa hutoweza basi ukiwa umelalia ubavu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alimuijia Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake mtu kipofu, Akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika sina muongozaji wa kuniongoza njia kuja msikitini, akamuomba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake amruhusu aswalie nyumbani kwake, akamruhusu, alipogeuka kuondoka akamuita, kisha akasema: Je unasikia wito wa swala? Akasema: Ndiyo, akasema: basi itikia wito wa sala.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapokuja mmoja wenu katika swala na imamu akawa yuko katika hali fulani, basi na afanye kama anavyofanya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alitufundisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Hotuba ya haja: Hakika kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, tunamtaka msaada na tunamuomba msamaha, na tunajilinda kwake kutokana na shari ya nafsi zetu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna ndoa bila walii (msimamizi)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayemuua aliyechukua ahadi ya kulindwa, hatonusa harufu ya pepo, na hakika hurufu yake hupatikana kuanzia mwendo wa miaka arobaini.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amemlaani Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake- mtoa rushwa na mpokea rushwa katika hukumu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Umejengwa uislamu kwa mambo matano
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kutosheka na mambo ya wajibu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Twahara (usafi) ni sehemu ya imani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapo sema Muadhini: Allahu Akbaru Allahu Akbaru, kisha akasema mmoja wenu: Allahu Akbaru Allahu Akbaru
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayeisahau swala, basi aiswali atakapoikumbuka, haina kafara nyingine isipokuwa hiyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika kilicho kati ya mtu na ushirikina na ukafiri ni kuacha swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika ahadi iliyopo kati yetu na wasiokuwa waislamu ni sala, na atakayeiacha sala basi huyo ni kafiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ibada ya Umra ndani ya ramadhani inalingana na Hija -au Hija pamoja nami.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akikaa itikafu katika kila ramadhani siku kumi, ulipofikia mwaka aliofishwa ndani yake alikaa itikafu siku ishirini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kwenu nyinyi jihadi bora: ni hija njema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba mwanamke mmoja alipatikana katika baadhi ya vita vya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akiwa kauwawa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimuendea Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Nikasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Hakika sisi tuko katika ardhi ya watu wa kitabu, je tule katika vyombo vyao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amekataza kuweka nadhiri, na akasema: Hakika nadhiri haiji kwa kheri, na hakika hutolewa kwayo (vilivyo) kwa bahili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mimi ninamuapa Mwenyezi Mungu -In shaa Allah- si api juu ya kiapo, nikaona kingine ni bora kuliko hicho isipokuwa nitaleta kilicho bora, na ninajivua nacho
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
La kwanza litakalohukumiwa kati ya watu siku ya kiyama ni katika damu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayepigana ili liwe neno la Mwenyezi Mungu ndio la juu basi huyo yuko katika njia ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakaye apa juu ya kiapo cha mila isiyokuwa ya uislamu kwa uongo tena kwa makusudi basi atakuwa kama alivyosema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtakapomsikia muadhini basi semeni mfano wa jinsi anavyosema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika safari, nikanyoosha mikono ili nimvue viatu vyake (khufu), akasema; ziache; kwani hakika mimi nimezivaa zikiwa safi, akafuta juu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba Fatuma bint Abii Hubaishi: Alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Akasema: Hakika mimi napata hedhi na wala sitwahariki, je niache swala? Akasema: Hapana usiache sala, Hakika huo niupasukaji wa mshipa, lakini acha swala kiasi cha siku ambazo ulikuwa ukiingia katika hedhi, kisha oga na uswali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nyoosheni safu zenu, kwani hakika kunyoosha safu ni katika ukamilifu wa swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapotawadha mmoja wenu basi na aweke puani mwake maji, kisha apenge, na atakayestanji kwa mawe basi ayafanye kuwa witiri, na atakapoamka mmoja wenu toka usingizini mwake basi na aoshe mikono yake kabla hajaiingiza katika chombo mara tatu, kwani hakika mmoja wenu hajui ni wapi ulilala mkono wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika dunia ni tamu, ni ya kijani, na hakika Mwenyezi Mungu anakumilikisheni ndani yake aone ni namna gani mtafanya, iogopeni dunia na waogopeni wanawake; kwani hakika fitina ya kwanza ya wana wa Israeli ilikuwa kwa wanawake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilisali pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- rakaa mbili kabla ya adhuhuri, na rakaa mbili baada yake, na rakaa mbili baada ya Ijumaa, na rakaa mbili baada ya magharibi, na rakaa mbili baada ya ishaa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapoamka asubuhi anasukutua kinywa chake kwa mswaki
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Paliletwa mashtaka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuhusu mtu anayepata wasiwasi kuwa anapata kitu ndani ya swala (katika vitenguzi vya udhu), Akasema: asiondoke mpaka asikie sauti, au apate harufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Itakaposimamishwa swala na kikatengwa chakula cha usiku basi anzeni na chakula cha usiku
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hachukii muumini wa kiume tabia za muumini wa kike, akichukia tabia fulani basi ataridhishwa na tabia nyingine. Au alisema:tofauti na hiyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akaenda haja ndogo, akatawadha, na akafuta juu ya khufu zake (viatu vya ngozi mfano wa soksi).
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtakapokwenda haja kubwa, msielekee kibla kwa haja kubwa wala ndogo, na wala msikipe kibla mgongo, lakini elekeeni mashariki au magharibi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asishike mmoja wenu utupu wake kwa mkono wake wa kulia akiwa anakidhi haja ndogo, na asijifute haja ndogo au kubwa kwa mkono wake wa kulia na asipumulie ndani ya chombo anachonywea.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amekataza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuswali baada ya swala ya sub-hi mpaka lichomoze jua, na baada ya laasiri mpaka lizame
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hivi haogopi mmoja wenu anayenyanyua kichwa chake kabla ya imamu Mwenyezi Mungu kukigeuza kichwa chake kuwa kichwa cha punda, au aifanye sura yake kuwa sura ya punda?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akinyanyua mikono yake usawa wa mabega yake anapofungua swala, na anapotoa takbira ya kurukuu, na anaponyanyua kichwa chake kutoka katika rukuu anainyanyua pia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alinifundisha mimi Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- tashahudi (tahiyatu), mkono wangu ukiwa katikati ya mikono yake kama anavyonifundisha sura katika Qur'ani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akiomba: Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwako kutokana na adhabu za kaburi, na adhabu ya moto, na mitihani ya uhai na kifo, na fitina za masihi dajali.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nimuweka fidia baba yangu na mama yangu, Hebu nieleze kunyamaza kwako kati ya takbira na kisomo: Ni nini unasema: Akasema: Ninasema: Allaahumma baaid bainiy -Ewe Mwenyezi Mungu weka mbali baina yangu- wa baina khatwaayaaya -na baina ya makosa yangu- kamaa baa a'tta bainal mashriqi wal maghribi -kama ulivyoweka mbali baina ya mashariki na magharibi. Allaahumma naqqiniy- Ewe Mwenyezi Mungu nitakase mimi- min khatwaayaaya -kutokana na makosa yangu- kamaa yunaqqaath-thaubul abyadhwa -kama inavyotakaswa nguo nyeupe- minad danasi -kutokana na uchafu. Allaahumma ghsilniy -Ewe Mwenyezi Mungu nioshe mimi- min khatwaayaaya -kutokana na makosa yangu- bil maai wath thalji wal baradi -kwa maji na barafu na baridi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Linganeni sawa katika sijida, na asikunjue mmoja wenu mikono yake kama anavyokunjua mbwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimuuliza Anas bin Malik: alikuwa Nabii Rehema na amani za Allah ziwe juu yake- akiswali na viatu vyake? akasema: ndio
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapokunywa mbwa katika chombo cha mmoja wenu basi akioshe mara saba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwako kutokana na mashetani wa kiume na mashetani wa kike.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayemuomba Mwenyezi Mungu shahada (yaani kufa shahidi) kwa ukweli, basi atamfikisha daraja ya mashahidi hata kama atafia juu ya godoro lake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Waliamrishwa watu kuwe kuagana kwao kwa mwisho ni katika nyumba (Alka'ba), isipokuwa likaondoshwa hilo kwa mwanamke mwenye hedhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kiliwekwa kwaajili ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- chombo cha kuogea janaba, akamimina kwa mkono wake wa kulia juu ya mkono wake wa kushoto mara mbili -au tatu- kisha akaosha tupu yake, kisha akapiga ardhi kwa mkono wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapooga janaba, anaosha mikono yake kisha anatawadha udhu wake wa swala kisha anaoga
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, wala nyumba zenu kuwa makaburi, na nitakieni rehma, kwani dua zenu hunifikia popote mlipo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa ni mtu mwenye madhii mengi, nikaona haya kumuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwasababu ya nafasi ya binti yake kwangu, nikamtuma Mikidadi bin Aswadi akamuuliza, akasema: Ataosha tupu yake, na atatawadha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtakapo vaa, na mtakapo tawadha, basi anzeni na kuliani kwenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ni amali ipi inayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu? Akasema: Ni (kuiswali) swala kwa wakati wake. Nikasema: kisha nini? Akasema: Ni kuwatendea wema wazazi wawili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ni nini kinachowaogopesha hawa? wanapatwa na ulaini (wanazikubali) katika aya zilizo wazi, na wanaangamia katika aya zinazotatiza
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna siku ambayo wanaamka ndani yake waja isipokuwa kuna Malaika wawili wanateremka,anasema mmoja wao: Ewe Mwenyezi Mungu mpe mtoaji badala,na anasema mwingine:Ewe Mwenyezi Mungu mpe mzuiaji hasara
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa kwa Saidi bin Jubair akasema: Ni nani kati yenu aliyeiona nyota iliyodondoka jana usiku? Nikasema: Mimi, kisha nikasema: Ama mimi sikuwa katika swala, lakini niling'atwa (na Nge)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nitampa bendera kesho mtu ambaye anampenda Allah na Mtume wake,na anapendwa na Allah na Mtume wake,kupitia yeye Allah ataleta ushindi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakaye muandaa mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu basi na yeye atakuwa kapigana, na atakayemsimamia mpiganaji katika familia yake basi na yeye atakuwa kapigana
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimshuhudia Amru bin Abii Hasan alimuuliza Abdullah bin Zaidi kuhusu udhu wa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akaagiza bakuli la maji, akatawadha kwaajili yao udhu wa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hivi hukujua kuwa uislamu hufuta madhambi yaliyokuwa kabla yake, na kuwa kuhama kunafuta madhambi yaliyokuwa kabla yake, nakuwa Hija inafuta madhambi yaliyokuwa kabla yake?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimjia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- naye akiwa anapiga mswaki kwa mswaki wa mti mbichi, Akasema: na ncha ya mswaki ikiwa katika ulimi wake, naye akisema: AAGH, AAGH (sauti ya kujigogoa), na mswaki ukiwa mdomoni mwake, kana kwamba anajigogoa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika inakutosheleza kusema kwa mikono yako hivi: kisha akapiga kwa mikono yake miwili chini ya ardhi mpigo mmoja, kisha akapaka mkono wa kulia kwa kutumia mkono wa wa kushoto, na akapaka juu ya viganja vyake na uso wake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Na hakuna Nabii aliyetumwa na Mwenyezi Mungu katika umma wowote kabla yangu, isipokuwa anakuwa katika umma wake na watu wake wapendwa na watu wanaoyachukua mafundisho yake na wanafuata amri yake, kisha wanakuja kutofautiana baada yao watu wanaowafuata, wanazungumza yale wasiyoyafanya, na wanafanya ambayo hawakuamrishwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na mguu wake ukiwa tayari umeuweka kwenye kipandwa (yaani yuko tayari kwa safari): Ni jihadi ipi bora? Akasema: ni neno la haki kwa kiongozi muovu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimpa utiifu Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- juu ya kusimamisha swala, na kutoa zaka, na kumnasihi kila muislamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mu'adhi, Wallahi hakika mimi ninakupenda, kisha ninakuusia ewe Mu'adhi, hakikisha usiache mwisho wa kila swala kusema: Allaahumma ainniy alaa dhikirika -Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie mimi niweze kukutaja wewe, Washukurika- na kukushukuru, Wahusni ibaadatika -Na kuzifanya vizuri ibada zako.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Adhabu kali ya moto itazipata nyayo za miguu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alichelewesha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- swala ya ishaa, akatoka Omar, akasema: Swala Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, wamelala wanawake na watoto, akatoka na kichwa chake kikitona maji akisema: Lau kama nisingehofia kuwapa tabu umma wangu basi ningewaamrisha swala hii waiswali wakati huu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amesema Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka-: Kila amali ya mwanadamu hiyo ni ya kwake isipokuwa swaumu, bila shaka hiyo ni yangu na mimi ndiye ninayeilipa.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Simama na uswali witiri ewe Aisha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Allaahumma inni Audhubiridhwaaka min sakhatwika, -Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwa radhi zako kutokana na hasira zako, wabimuaafaatika min uquubatika,- Na kwa msamaha wako kutokana na adhabu zako-, Wa a'udhubika minka, -na ninajilinda kwako kwa ulinzi utokao kwako-, Laa uhswith thanaa 'alaika, -Siwezi kuzidhibiti shukurani zote juu yako, Anta kamaa athnaita a'laa nafsika, -Wewe kama ulivyojisifia nafsi yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Aliulizwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: Ni swala ipi bora? Akasema: Ni kurefusha kisimamo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ni kwa jambo lipi alikuwa akianza nalo Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Anapoingia nyumbani kwake? Akasema: kwa mswaki
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Huyo mtu kamkojolea shetani masikioni mwake, au alisema: sikioni kwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mambo kumi ni katika maumbile: Kupunguza masharubu, na kuziachia ndevu,na kupiga mswaki, na kupandisha maji puani, na kupunguza kucha, na kuosha fundo za vidole, na kunyofoa nywele za makwapani, na kunyoa nywele za sehemu za siri, na kustanji kwa maji.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Anafunga shetani juu ya kisogo cha kichwa cha mmoja wenu, pindi anapolala, mafundo matatu, anapiga katika kila fundo: Unatakiwa kulala usiku mrefu basi lala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Shikamana na kukithirisha kusujudu; kwani wewe hutosujudu kwaajili ya Mwenyezi Mungu sijida moja isipokuwa atakunyanyua Mwenyezi Mungu kwa hiyo sijida daraja moja, na anakufutia kwa hiyo dhambi moja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akifanya juhudi katika ramadhani kwa namna ambayo hajitahidi katika nyakati zingine nje ya ramadhani, na katika kumi la mwisho pia alikuwa na juhudi ambazo hakuwa anajitahidi hivyo nje ya ramadhani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Tulikuwa tukimuandalia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- mswaki wake na (maji yake kwaajili ya) twahara, basi Mwenyezi Mungu anamuamsha kwa muda anaotaka aamke nyakati za usiku, anapiga mswaki, na anatawadha na anaswali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haijawahi kupata vumbi miguu ya mja yeyote katika njia ya Mwenyezi Mungu, halafu ikaguswa na moto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Anachokipata aliyekufa shahidi katika maumivu ya kifo, ni kama maumivu anayoyapata mmoja wenu kutokana na kung'atwa na mdudu chungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayependa Mwenyezi Mungu amuokoe na Matatizo ya siku ya kiyama, basi amtatulie shida mwenye ugumu au ampunguzie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayeswali (katika nyakati mbili) za baridi ataingia peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hivi unaonaje ikiwa nitauwawa katika njia ya Mwenyezi Mungu, je yatafutwa makosa yangu?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Swala ya mtu katika jamaa inazidi swala yake sokoni kwake na nyumbani kwake kwa daraja zaidi ya ishirini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hebu nielezeni lau kama Mto ungelikua mlangoni kwa mmoja wenu akioga humo kila siku mara tano, unasemaje kuhusu hilo, kunaweza kubaki na uchafu katika mwili wake?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Waamrisheni watoto wenu kuswali nao wakiwa watoto wa miaka saba, na wapigeni kwa ajili yake nao wakiwa watoto wa miaka kumi, na watenganisheni baina yao katika malazi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mtume rehema na amani ziwe juu yake alitoka kwetu sisi, tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tumekwishafahamu ni vipi tutakusalimu, sasa ni vipi tutakutakia Rehema?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hana swala yeyote ambaye hakusoma sura kifunguzi cha kitabu (suratul faatiha)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kila mmoja miongoni mwenu ni mchunga hivyo ataulizwa kuhusu raia wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna Muislamu yeyote atafikiwa na Sala ya lazima kisha akaufanya vizuri udhu wake, na Unyenyekevu wake na Rakaa zake, isipokuwa inakuwa ni kifuta madhambi yaliyo kuwa kabla ya Sala, kwa muda ambao hajafanya madhambi makubwa, na hivyo ndivyo ilivyo kila siku
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Adh-kari za baada ya sala ya faradhi hapati hasara msomaji au mfanyaji wake, kusema Sub-haana llahi mara thelathini na tatu (33), Al-hamdulillahi mara thelethini na tatu (33), Allahu Akbaru mara thelathini na nne (34)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayesema wakati anamsikia muadhini: Ninashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika nakuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake, nimeridhia kuwa Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na Muhammadi kuwa ni Mtume na Uislamu kuwa ni dini, atasamehewa dhambi zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba mtu mmoja alitawadha, akaacha sehemu ndogo saizi ya kucha miguuni kwake, akaiona Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akasema: "Rudi katawadhe vizuri udhu wako" Akarudi, kisha akaswali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Tulikuwa hatuchukulii maji maji ya kahawia na njano baada ya twahara kuwa ni chochote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kaa kiasi cha siku ambazo ilikuwa ikidumu hedhi yako, kisha oga
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kuoga siku ya Ijumaa ni wajibu kwa kila aliyebaleghe, na apige mswaki, na aguse marashi ikiwa atapata
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asisafiri mwanamke mwendo wa siku mbili mpaka awe pamoja na mume wake, au maharimu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Matendo yapo ya aina sita na watu wapo wako aina nne, basi kuna watu wa aina mbili wanaostahiki malipo, na malipo yao huwa sawa na matendo yao, na jema moja hulipwa kwa kumi mfano wake, na jema moja huzidishwa mpaka kufikia mema mia saba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kwa hakika Mwenyezi Mungu anapenda ichukuliwe ruhusa yake katika kufanya yaliyo mepesi, kama vile anavyopendelea kwa waja wake kufanya mambo yake aliyowawajibishia kuyafanya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenyezi Mungu akimpangia mja afie sehemu fulani humfanya ahitajie kitu sehemu ile
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
na mimi ndiye ninaitwa Dhwamam Bin Thaalaba ndugu wa Banii Saad Bin Bakri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kila wakati wa swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alitawadha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mara moja moja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Anasimulia kuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alitawadha mara mbili mbili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapo hisi mmoja wenu chochote tumboni kwake, akapata wasi wasi, je kuna chochote kimemtoka au la?, basi asitoke msikitini mpaka asikie sauti, au anuse harufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ni haki kwa kila muislamu aoge katika kila siku saba walau siku moja, aoshe ndani yake kichwa chake na mwili wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilimwendea Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- nikitaka kuwa muislamu, akaniamrisha nioge kwa maji na mkunazi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtakapo msikia muadhini basi semeni mfano wa yale anayo yasema, kisha mnitakie rehema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayejenga msikiti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu atamjengea Peponi nyumba mfano wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kusali ndani ya Msikiti wangu huu ni bora kuliko sala elfu moja zinazo swaliwa nje ya Msikiti huu isipokuwa Msikiti wa Makka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi asali rakaa mbili kabla hajakaa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi aseme: Allaahummaf-tah lii abwaaba rahmatika (Ewe Mola wangu, nifungulie milango ya rehema zako), na akitoka aseme: Allaahumma innii as-aluka min fadhlika (Ewe Mola wangu ninakuomba unipe katika fadhila zako)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Bilali, simamisha swala, tupe raha kwayo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Enyi watu! Bila shaka nimefanya hivi ili muige na mjifunze swala yangu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Pindi mtakaposwali basi nyoosheni safu zenu, kisha akuongozeni mmoja wenu, atakapotoa takbira basi toeni takbira
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hakika mimi ndiye mtu niliyekaribu zaidi kwenu nyinyi swala yangu kufanana na swala ya Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, bila shaka hii ndio ilikuwa swala yake mpaka alipoondoka duniani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwizi mbaya zaidi kuliko watu wote, ni yule anayeiba swala yake" Akasema: Ataiba vipi swala yake? Akasema: "Hatimizi rukuu zake wala sijida zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- anaponyanyua mgongo wake kutoka katika rukuu anasema: "Sami'allaahu liman hamidah
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikua akisema mwishoni mwa kila swala ya faradhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema kati ya sijida mbiliL "Rabbigh-firlii, Rabbigh-firlii
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Huyo ni Shetani anaitwa Khinzab, ukimuhisi basi haraka sana taka ulinzi kutoka kwa Allah dhidi yake, na uteme kushotoni kwako mara tatu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakaetubebea silaha, si miongoni mwetu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa