عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: "إن الرقى والتمائم والتِّوَلَة شرك".
[صحيح] - [رواه أبو داود وابن ماجه وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillah bin Masudi-Radhi za Allah ziwe juu yake- Amesema: Nilimsikia Mtume -Rehma na amani ziwe juu yake- " Akisema: "Hakika makombe na mahirizi na limbwata ni ushirikina"
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah
Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake anaeleza kuwa kutumia vitu hivi kwa lengo la kuzuia madhara na kuleta maslahi kutoka kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu, kwasababu hakuna anayemiliki kuzuia madhara wala kuleta kheri ispokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na habari hii maana yake ni katazo la kitendo hiki. Makombe -na pia huitwa maazima- nayo ni yale yanayotundikwa kwa watoto miongoni mwa hirizi na mfano wake, Na Limbwata nalo ni lile linalotengenezwa kwaajili ya kumfanya mmoja kati ya wanandoa ampende mwenzake kuwa haya ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kinachofaa katika makombe ni lile lililoambatana na sharti tatu: Ya kwanza: Asiitakidi kuwa linauwezo wa kunufaisha lenyewe bila Mwenyezi Mungu, ikiwa ataitakidi kuwa linanufaisha lenyewe bila Mwenyezi Mungu basi hilo ni haramu, bali ni shirki, bali aitakidi kuwa lenyewe ni sababu haliwezi kunufaisha ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, Sharti la pili: Lisiwe katika yale yanayokwenda kinyume na sheria, kama litakavyokuwa limeambatana na kumuomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu, au kutaka msaada kwa jini, na mfano wake, hilo ni haramu, bali ni shirki, Sharti la tatu: Liwe linafahamika na linaeleweka, ikiwa ni katika aina za talasimu na mazingaombwe, basi hilo haliruhusiwi.