عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: «ما نهيتكم عنه فاجتنبوه، وما أمرتكم به فأْتُوا منه ما استطعتم، فإنما أَهلَكَ الذين من قبلكم كثرةُ مسائلهم واختلافهم على أنبيائهم».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Nilimsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema: "Niliyokukatazeni basi yaepukeni, na yale niliyokuamrisheni basi yaleteni katika hayo kadiri muwezavyo, na hakika waliangamia wale waliokuwa kabla yenu, kwa kukithiri maswali yao, na kuhitilafiana kwao na Manabii wao".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Ametuelekeza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake yakwamba yeye anapotukataza kitu ni wajibu kwetu kukiepuka bila kubagua, na akituamrisha chochote ni juu yetu kukifanya kwa kadiri tuwezavyo. Kisha akatutahadharisha ili tusijekuwa kama umma zilizotangulia pindi walipokithirisha maswali juu ya Manabii wao pamoja nakwenda kwao kinyume nao, akawaadhibu Mwenyezi Mungu kwa aina mbalimbali za maangamivu na adhabu, tunatakiwa tusiwe mfano wao ili tusiangamie kama walivyoangamia.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani Pashto Kiassam Albanian
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Amri ya kutekeleza maamrisho, na kuyaepuka makatazo.
  2. Katazo halikuruhusu kufanya kitu chochote miongoni mwa hivyo, na amri ikawekewa sharti la kuweza; kwasababu kuacha ni jambo linawezekana na kufanya ni jambo linahitaji uwezo wa kukileta kitendo kilichoamrishwa.
  3. Katazo la kukithirisha maswali, wameyagawanya wanachuoni maswali katika sehemu mbili: Ya kwanza: Ni yale yanayokuwa katika mfumo wa kujifunza katika mambo yanayohitajika miongoni mwa mambo ya dini, haya yameamrishwa, na miongoni mwa hayo ni maswali ya maswahaba. Na ya pili: Ni yale yanayokuwa katika mfumo wa ukaidi na kulazimisha, na haya ndiyo yaliyokatazwa.
  4. Kutahadharishwa umma huu na kutokwenda kinyume na Nabii wake, kama ilivyotokea katika umma zilizokuwa kabla yake.
  5. Katazo lake linajumuisha kidogo na kingi, kwasababu haiwezi kufikia kuyaepuka makatazo ispokuwa kwa kuyaepuka yale madogo na mengi, kwa mfano: Ametukataza kula riba, katazo linajumuisha kidogo na kingi.
  6. Kuziacha sababu zote zinazopelekea katika mambo ya haramu, kwasababu kufanya hivyo ni miongoni mwa maana za kuyaepuka.
  7. Mwanadamu ana nguvu na uwezo, kwa kauli yake: "Kwa kiasi muwezavyo" ndani ya kauli hii ni jibu la madhehebu ya Jabariyya wanaosema kuwa: mwanadamu hana uwezo, kwasababu yeye amelazimishwa juu ya matendo yake, hata pale mtu anapotikisa mkono wake wakati wa mazungumzo, wanasema kutikisa mkono huku si kwa uwezo wake, bali kalazimishwa, na hakuna shaka kuwa kauli hii ni batili na inaambatana na madhara makubwa.
  8. Haitakiwi kwa mwanadamu anaposikia amri ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake aseme: Kwani hiyo ni wajibu au ni sunna? kwa kauli yake: "Lifanyeni kwa kadiri muwezavyo".
  9. Yote aliyoyaamrisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- au akayakataza basi hiyo ni sheria, swasawa hilo liwe ndani ya Qur'ani au lisiwemo, itafanyiwa kazi sunna ya ziyada katika Qu'r'ani iwe amri au katazo.
  10. Kukithirisha maswali ni sababu ya kuangamia, hasa hasa katika mambo ambayo haiwezekani kuyafikia, mfano kama maswala ya ghaibu kama majina ya Mwenyezi Mungu na sifa zake, na hali za siku ya kiyama, usikithirishe maswali ndani yake ukaangamia, ukawa ni mtu mwenye kulazimisha mambo mwenye kujikita.
  11. Umma waliotangulia waliangamia kwa kukithiri maswali yao, na waliangamia kwa kukithiri kwenda kwao kinyume na Manabii wao.