عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضيَ اللهُ عنه قَالَ:
جَاءَ رَجُلٌ إِلَى رَسُولِ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ، أَرَأَيْتَ إِنْ جَاءَ رَجُلٌ يُرِيدُ أَخْذَ مَالِي؟ قَالَ: «فَلَا تُعْطِهِ مَالَكَ» قَالَ: أَرَأَيْتَ إِنْ قَاتَلَنِي؟ قَالَ: «قَاتِلْهُ» قَالَ: أَرَأَيْتَ إِنْ قَتَلَنِي؟ قَالَ: «فَأَنْتَ شَهِيدٌ»، قَالَ: أَرَأَيْتَ إِنْ قَتَلْتُهُ؟ قَالَ: «هُوَ فِي النَّارِ».
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 140]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema:
Alikuja mtu mmoja kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hivi wasemaje endapo atakuja mtu anataka kuchukua mali yangu? Akasema: "Usimpe mali yako" Akasema: Wasemaje kama akipigana nami? Akasema: "Pigana naye" Akasema: Wasemaje kama ataniuwa? Akasema: "Basi utakuwa umekufa shahidi". Akasema: Wasemaje kama nitamuuwa? Akasema: "Huyo ataingia Motoni".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 140]
Alikuja mtu mmoja kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, wasemaje endapo atakuja mtu akataka kuchukua mali yangu? Akasema: Hutakiwi kujisalimilisha kwake na ukampatia mali yako, akasema: Wasemaje akipigana nami? Akasema: Inafaa kwako kupigana naye, akasema: Wasemaje endapo ataniuwa? Akasema: Basi wewe utakuwa shahidi, akasema: Wasemaje endapo nikimuuwa? Akasema: Basi yeye atastahiki kuadhibiwa motoni siku ya Kiyama.