عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «الكبائر: الإشراك بالله، وعُقُوق الوالدين، وقتل النفس، واليمين الغَمُوس».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillaahi bin Amri bin Aaswi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Kutoka kwa Mtume rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Madhambi makubwa: Ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu, na kuwaasi wazazi wawili, na kuuwa nafsi, na kiapo cha uongo"
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Inakusanya hadithi hii idadi kadhaa ya madhambi ambayo yamesifiwa kuwa ni katika makubwa, na yameitwa hivyo kwasababu ya ukubwa wa madhara yake kwa mfanyaji wake na kwa watu duniani na Akhera. La kwanza: "Ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu": Yaani: ni kumkufuru Mwenyezi Mungu kwa: kuabudu pamoja naye mwingine, na akakanusha ibada za Mola wake. La pili: "Kuwaasi wazazi wawili" Na uwasi uhakika wake: Ni afanye akiwa na wazazi wake wawili au mmoja kati yao, yatakayo wachukiza kimazoea, kama kutowaheshimu na kuwatukana na kutowahudumia na kuwaangalia pale wanapomuhitaji mtoto. Na la tatu: "Ni kuuwa nafsi" bila hatia kama kuuwa kwa dhulma na uadui, ama akistahiki mtu kuuawa kwa haki kama kisasi na vinginevyo haitoingia katika maana ya hadithi hii. Kisha ikahitimishwa hadithi kwa kuhofisha kutokana na "kiapo cha uongo" na kimeitwa kuwa ni cha uongo yaani (kiapo kinacho zamisha) kwasababu kinamzamisha mwenye kuapa katika madhambi au motoni; kwasababu yeye ameapia uongo hali yakuwa anajua kuwa ni uongo.