عن أبي بكر الصديق رضي الله عنه قال: ارْقَبُوا محمَّدًا -صلَّى اللهُ عليهِ وسلَّم- فِي أَهلِ بَيتِهِ.
[صحيح موقوفًا على أبي بكر الصديق -رضي الله عنه] - [رواه البخاري من قول أبي بكر -رضي الله عنه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuubakri Al-sswiddiq -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Mchungeni(mfuatilieni)Muhammadi -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa watu wa nyumba yake.
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Katika nukuu ya maneno ya Abuubakari -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuna ushahidi wa uelewa wa maswahaba -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- wa haki za watu wa familia ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Na kuwatukuza kwao na kuwaheshimu kwao, yeyote atakayekuwa ni katika watu wa familia yake na akawa kanyooka katika dini na mwenye kufuata sunna za Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- basi huyo ana haki mbili: Haki ya uislamu na haki ya udugu wa karibu na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na nikuwa Abuubakari na maswahaba wengine walikuwa wakiwapenda watu wa nyumba ya Mtume na wakiusia kutendewa mazuri.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama