عن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما مرفوعاً: «إِذَا دَخَل الرَّجُل بَيتَه، فَذَكَرَ اللهَ -تَعَالَى- عِندَ دُخُولِهِ، وَعِندَ طَعَامِهِ، قَالَ الشَّيطَانُ لِأَصْحَابِهِ: لاَ مَبِيتَ لَكُم وَلاَ عَشَاءَ، وَإِذَا دَخَلَ فَلَم يَذْكُر الله -تَعَالَى- عِندَ دُخُولِهِ، قَالَ الشَّيطَان: أَدْرَكْتُمُ المَبِيت؛ وَإِذا لَمْ يَذْكُرِ اللهَ -تَعَالَى- عِندَ طَعَامِه، قالَ: أَدرَكتُم المَبِيتَ وَالعَشَاءَ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jabir bin Abdillah -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakapoingia mtu nyumbani kwake, akamtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa kuingia kwake na wakati wa kula kwake husema shetani kuwaambia jamaa zake: Hamna malazi wala chakula cha usiku kwenu, na atakapoingia akawa hakumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa kuingia kwake, shetani husema: mmepata malazi na chakula cha usiku"
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Hadithi ya Jabir -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- imekuja katika maudhui ya adabu za chakula, kiasi kwamba ameeleza -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- amesema: "Atakapoingia mtu nyumbani kwake, akamtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa kuingia kwake na wakati wa kula kwake husema shetani kuwaambia jamaa zake: Hamna malazi wala chakula cha usiku kwenu"; Na hii ni kwasababu mtu kamtaja Mwenyezi Mungu. Na kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa kuingia nyumbani ni aseme: "Bismillaahi walaj-naa, Wa bismillaahi Kharajinaa, wa a'laa Rabbinaa Tawakkal-naa, Allaahumma innii as-aluka khairal mauliji wa khairal makhraji" Yaani: (kwa jina la Mwenyezi Mungu tumerejea, na kwa jina la Mwenyezi Mungu tulitoka, na kwa Mola wetu ndiko tunakotegemea, Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba kheri ya kutoka na kheri ya kurejea", kama ilivyokuja katika hadithi ambayo imekatika katika isnadi yake (mlolongo wa wapokezi wake), na ama kumtaja Mwenyezi Mungu wakati wa kula ni aseme: "Bismillaahi" Yaani: (Ninaanza kwa jina la Mwenyezi Mungu). Atakapomtaja Mwenyezi Mungu wakati wa kuingia kwake nyumbani, na akamtaja Mwenyezi Mungu wakati wa kula kwake chakula cha usiku, shetani husema kuwaambia watu wake: "Hamna malazi kwenu nyinyi wala chakula cha usiku"; kwasababu nyumba hii na chakula hiki cha usiku vimelindwa kwa kutajwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, Ameilinda Mwenyezi Mungu kutokana na mashetani. Na atakapoingia akawa hakumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa kuingia kwake, shetani husema: "mmepata malazi", na kinapotengwa kwake chakula na akawa hakumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu wakati wa chakula chake husema: "Mmepata malazi na chakula cha usiku" Yaani shetani hushirikiana naye malazi na chakula; kwa kutojilinda kwa kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na katika hadithi hii kuna himizo la kuwa mwanadamu anatakiwa atakapoingia nyumbani kwake ataje jina la Mwenyezi Mungu, na hivyo hivyo wakati wa chakula chake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama