عن أبي الدرداء رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «مَنْ رَدَّ عَنْ عِرْضِ أَخِيهِ رَدَّ اللَّهُ عَنْ وَجْهِهِ النَّارَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Dardaa -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Atakayerudisha heshima ya ndugu yake, basi Mwenyezi Mungu atauweka mbali uso wake na moto siku ya kiyama".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Katika hadithi kuna ubora wa atakayerudisha heshima ya ndugu yake muislamu, Anapomsengenya mmoja kati ya wale waliopo katika kikao, basi ni wajibu kwako kumtetea ndugu yako muislamu, na kumnyamazisha msengenyaji, na kukemea uovu, ama ukimuacha hii inahesabika ni kumsaliti ndugu yako muislamu, na kinachojulisha kuwa makusudio ya hilo ni kumsengenya ni hadithi ya Asmaa binti Yazidi, kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Atakayetetea nyama ya ndugu yake katika usengenywaji, basi ni haki kwa Mwenyezi Mungu kumuacha huru na moto" kaipokea Ahmad na kaisahihisha Al-baaniy.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Thawabu hizi ni maalumu katika hali ya kutokuwepo ndugu yako muislamu anayesengenywa.
  2. Nikuwa malipo huendana na matendo, atakayerudisha heshima ya ndugu yake ataurudisha Mwenyezi Mungu uso wake kutoingia motoni.
  3. kuthibitisha moto na kuthibitisha kiyama kuwa vipo.