عن أبي الدرداء رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «مَنْ رَدَّ عَنْ عِرْضِ أَخِيهِ رَدَّ اللَّهُ عَنْ وَجْهِهِ النَّارَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Dardaa -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Atakayerudisha heshima ya ndugu yake, basi Mwenyezi Mungu atauweka mbali uso wake na moto siku ya kiyama".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy
Katika hadithi kuna ubora wa atakayerudisha heshima ya ndugu yake muislamu, Anapomsengenya mmoja kati ya wale waliopo katika kikao, basi ni wajibu kwako kumtetea ndugu yako muislamu, na kumnyamazisha msengenyaji, na kukemea uovu, ama ukimuacha hii inahesabika ni kumsaliti ndugu yako muislamu, na kinachojulisha kuwa makusudio ya hilo ni kumsengenya ni hadithi ya Asmaa binti Yazidi, kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Atakayetetea nyama ya ndugu yake katika usengenywaji, basi ni haki kwa Mwenyezi Mungu kumuacha huru na moto" kaipokea Ahmad na kaisahihisha Al-baaniy.