عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «ما نقصت صدقة من مال، وما زاد الله عبدا بعفو إلا عزا، وما تواضع أحد لله إلا رفعه الله عز وجل »
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake yakwamba Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Haijawahi kupunguza sadaka chochote katika mali, Na hajawahi kumzidishia Mwenyezi Mungu mja kwa usamehevu (wake) ispokuwa utukufu, na hajawahi kunyenyekea yeyote ispokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu alimnyanyua".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

(Haijawahi kupunguza sadaka chochote katika mali) Maana yake nikuwa: sadaka inapotolewa basi haipunguzi mali bali inaizidisha, na inaitia baraka, na inaizuilia maafa, kuzidi kwa mali ima kiwango: kwa kumfungulia Mwenyezi Mungu mja milango ya riziki, au namna: kwa kuiteremshia Mwenyezi Mungu baraka ambayo inaizidisha kwa kadiri ya kile alichokitoa katika sadaka. Na hamuongezei Mwenyezi Mungu mja kwa usamehevu wake ispokuwa utukufu, yaani: nikuwa mwenye kujua faida za kusamehe na akaacha kuadhibu na kulaumu, basi atapata heshima na utukufu katika nyoyo, na ataongeza utukufu na karama, na kupandishwa daraja duniani na akhera. Na hajawahi kunyenyekea mja kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ispokuwa Mwenyezi Mungu humnyanyua, Maana yake nikuwa mwenye kujidhalilisha kwa Mwenyezi Mungu na akaonyesha unyonge mbele yake Aliyetakasika na kutukuka, na akawa mlaini katika upande wa viumbe, na akaonyesha unyonge kwa waislamu, basi sifa hizi hazimuongezei mwenye kujipamba nazo ispokuwa ni kunyanyuliwa daraja duniani na akhera na mapenzi katika nyoyo, na nafasi ya juu peponi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuhimizwa juu ya sadaka.
  2. Nikuwa sadaka ni sababu ya kuilinda mali na kuikuza na kuitia baraka.
  3. Kuongezeka katika mali kunaweza kuwa kimaana (inayoonekana) kama Mwenyezi Mungu kumfungulia milango ya riziki, na kunaweza kuwa kihisia (kusikoonekana) kwa kushusha Mwenyezi Mungu baraka juu ya mali ikaongezeka kwa kadiri ya kile alichokitoa kwa ajili ya sadaka.
  4. Kuhimizwa juu ya kusamehe mabaya.
  5. Kuhimizwa juu ya unyenyekevu.
  6. Nikuwa unyenyekevu si udhalili kama wanavyodhani baadhi ya watu, bali ni utukufu kama alivyoeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.
  7. Hizi ni fadhila za unyenyekevu kwa atakayenyenyekea kwa kutaraji malipo kwa Mwenyezi Mungu nasi kwa kujionyesha (Atakayenyenyekea kwaajili ya Mwenyezi Mungu).
  8. Nikuwa utukufu na kunyanyuliwa daraja viko mkononi mwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, anampa amtakaye katika wale ambao zimepatikana kwao sababu zake.