عن أبي هريرة عبدالرحمن بن صخر الدوسي رضي الله عنه مرفوعاً: .«قال الله تعالى: أنفق يا ابن آدم ينفق عليك».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira- Abdur Rahmani bin Swakhari Ad-dusiy- Radhi za Mwenyzi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Toa ewe mwanadamu utapewa".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Toa utapewa, Yaani: usiogope umasikini kwa kutumia mali na kuzitoa, na wala usiwe bahili, kwani wewe unapotoa kumpa mwingine basi atakupa Mwenyezi Mungu, mlivyonavyo ni vyenye kumalizika na vilivyoko kwa Mwenyezi Mungu ni vyenye kubakia, na hadithi hii inamaanisha kauli yake Mtukufu: "Na hamtatoa chochote ispokuwa yeye hukirejesha" ikakusanya kuhimizwa juu ya kutoa katika njia za kheri, na kujipa matumaini ya kurejeshewa kutoka katika fadhila za Mwenyezi Mungu Mtukufu.