عن أبي هريرة عبدالرحمن بن صخر الدوسي رضي الله عنه مرفوعاً: .«قال الله تعالى: أنفق يا ابن آدم ينفق عليك».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira- Abdur Rahmani bin Swakhari Ad-dusiy- Radhi za Mwenyzi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Toa ewe mwanadamu utapewa".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Toa utapewa, Yaani: usiogope umasikini kwa kutumia mali na kuzitoa, na wala usiwe bahili, kwani wewe unapotoa kumpa mwingine basi atakupa Mwenyezi Mungu, mlivyonavyo ni vyenye kumalizika na vilivyoko kwa Mwenyezi Mungu ni vyenye kubakia, na hadithi hii inamaanisha kauli yake Mtukufu: "Na hamtatoa chochote ispokuwa yeye hukirejesha" ikakusanya kuhimizwa juu ya kutoa katika njia za kheri, na kujipa matumaini ya kurejeshewa kutoka katika fadhila za Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kutoa ni sababu ya kupanuliwa riziki.
  2. Kumpa Mwenyezi Mungu mja wake kulingana na utoaji wake kwa mja fukara na mwenye uhitaji.
  3. Hazina za Mwenyezi Mungu zimejaa mno wala hazimaliziki, na Mola ni mkarimu habanii kwa kuogopea umasikini.