عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا:
أَنَّ رَجُلًا سَأَلَ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: أَيُّ الإِسْلاَمِ خَيْرٌ؟ قَالَ: «تُطْعِمُ الطَّعَامَ، وَتَقْرَأُ السَّلاَمَ عَلَى مَنْ عَرَفْتَ وَمَنْ لَمْ تَعْرِفْ».

[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdallah Bin Amri -Radhi za Allah ziwe juu yake na baba yake-:
Ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ni, ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua".

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Aliulizwa Mtume rehema na amani zimfikie: Ni jambo lipi katika Uislamu ni bora? Akataja mambo mawili:
La kwanza: Kukirithirisha kuwalisha masikini, na inaingia hapa sadaka na zawadi na kuwakirimu wageni na walima (harusi), na inatiliwa mkazo fadhila ya kulisha masikini katika nyakati za njaa na wakati wa bidhaa kupanda bei.
La pili: Kumpa salamu kila muislamu, unayemjua na usiyemjua.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Pupa ya Masahaba katika kuyajua mambo yenye manufaa katika Dunia na Akhera.
  2. Salamu na kulisha chakula ni miongoni mwa amali bora katika Uislamu; kwa sababu ya fadhila zake na uhitaji wa watu juu ya chakula katika wakati wote.
  3. Kwa mambo haya mawili ihisani (wema) unakuwa kwa kauli na vitendo, nao ndio wema uliokamilika zaidi.
  4. Mambo haya ni katika mambo yanayohusu maisha ya waislamu baina yao, na kuna mambo yanahusu mahusiano ya mja na Mola wake.
  5. Kuanza kwa salamu ni maalumu kwa waislamu, haitolewi salamu kwa kumuanza asiyekuwa muislamu.