Orodha ya Hadithi

Atakapo mpenda mtu ndugu yake amwambie kuwa anampenda.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haki za Muislamu juu ya muislamu ni tano: Kujibu salamu, na kumtembelea mgonjwa, na kusindikiza jeneza, na kuitika wito, na kumtakia rehma mwenye kupiga chafya.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Je mnajua ni nini kusengenya? wakasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wajuzi, akasema: ni kumsema kwako ndugu yako kwa yale anayoyachukia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Si halali kwa muislamu kumhama ndugu yake zaidi ya siku tatu, wanakutana: huyu anampuuza huyu, na huyu anampuuza huyu, na mbora wao ni yule anayeanza kwa salamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hakatai marashi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu huridhika kwa mja anapokula chochote, akamshukuru juu ya hicho, au akanywa chochote akamshukuru juu ya hicho.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe kijana, mtaje Mwenyezi Mungu, na ule kwa mkono wako wa kulia, na ule chakula kilicho mbele yako" kinachokuelekea"
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapo kula mmoja wenu basi na ale kwa mkono wake wa kulia, na atakapo kunywa basi na anywe kwa mkono wake wa kulia, kwani shetani anakula kwa mkono wako wake wa kushoto, na anakunywa kwa mkono wake wa kushoto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msivae hariri nyepesi wala nguo zilizofumwa kwa hariri, na wala msinywe katika vyombo vya dhahabu wala fedha, na wala msile katika sahani zake, kwani hivyo ni vyao duniani na ni vyenu Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msivae hariri; kwani atakayeivaa duniani hatoivaa Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika safari, nikanyoosha mikono ili nimvue viatu vyake (khufu), akasema; ziache; kwani hakika mimi nimezivaa zikiwa safi, akafuta juu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Je anaweza kulala mmoja wetu akiwa na janaba? Akasema: Ndiyo, atakapotawadha mmoja wenu basi na alale
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapotawadha mmoja wenu basi na aweke puani mwake maji, kisha apenge, na atakayestanji kwa mawe basi ayafanye kuwa witiri, na atakapoamka mmoja wenu toka usingizini mwake basi na aoshe mikono yake kabla hajaiingiza katika chombo mara tatu, kwani hakika mmoja wenu hajui ni wapi ulilala mkono wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asishike mmoja wenu utupu wake kwa mkono wake wa kulia akiwa anakidhi haja ndogo, na asijifute haja ndogo au kubwa kwa mkono wake wa kulia na asipumulie ndani ya chombo anachonywea.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapoona mmoja wenu ndoto anayoipenda, basi hiyo imetoka kwa Mwenyezi Mungu, na amshukuru Mwenyezi Mungu juu yake, na aisimulie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapopiga chafya anaweka mkono wake au nguo yake juu ya kinywa chake, na anapunguza sauti yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mtakapo vaa, na mtakapo tawadha, basi anzeni na kuliani kwenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba mtu mmoja alikula kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa mkono wake wa kushoto, akasema: kula kwa mkono wako wa kulia, akasema: siwezi. akasema: Hutoweza, hakuna kilichomzuia isipokuwa ni kiburi, basi hakuweza tena kuunyanyua kufika kinywani kwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ni nani anayejiapiza kwangu kuwa sitomsamehe fulani? Hakika mimi nimemsamehe,na nimeyaporomosha matendo yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mja anaweza kuzungumza neno asilijali ndani yake akateleza kwa neno hilo nakuingia katika moto ambao umbali wake ni baina ya mashariki na magharibi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakapokutana mmoja wenu na ndugu yake basi na amsalimie, ukiwatenganisha kati yao mti, au ukuta, au jiwe, kisha akakutana naye tena basi amsalimie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ndoto nzuri hutoka kwa Mwenyezi Mungu, na njozi hutoka kwa shetani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Zuia ulimi wako, na ikutosheleze nyumba yako, na ulie juu ya makosa yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayependezwa na kumtazama mtu miongoni mwa watu wa peponi basi na amtazame huyu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Haijabakia katika utume isipokuwa viashiria vya habari njema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayeniona mimi ndotoni basi ataniona akiwa macho -au ni kana kwamba kaniona akiwa macho- hajifananishi shetani na mimi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Amsalimie aliyepanda anayetembea, na anayetembea aliyekaa, na wachache kwa wengi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna kitu chenye uzito zaidi katika mizani ya muumini siku ya Kiyama kuliko tabia njema, na hakika Mwenyezi Mungu anamchukia mtu muovu mwenye kauli chafu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mtume rehema na amani ziwe juu yake alitoka kwetu sisi, tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tumekwishafahamu ni vipi tutakusalimu, sasa ni vipi tutakutakia Rehema?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ni, ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Asiangalie mwanaume katika uchi wa mwanaume mwenzie, wala mwanamke kutazama uchi wa mwanamke mwenzie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Muislamu wa kweli ni yule wanayepata Amani waislamu wenzake kutokana na ulimi wake na mkono wake, na mhamaji ni yule mwenye kuyahama yale aliyoyakataza Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenye kuisoma Qur'ani kwa sauti ya wazi ni kama mwenye kutoa sadaka hadharani, na mwenye kuisoma Qur'ani kwa siri ni kama mwenye kuficha sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapolala kitandani kwake wakati wa kila usiku alikuwa akikusanya viganja vyake, kisha akivipuliza na kuvisomea : {Qul-huwallahu Ahad}, na {Qul-A uudhu birabbil falaq} na (Qul-Auudhu birabbi naas }
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa