عن أنس بن مالك رضي الله عنه مرفوعاً: أن النبي صلى الله عليه وسلم كان لا يَرُدُّ الطيب.
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas bin Maliki Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: Yakuwa, Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hakatai marashi.
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Ilikuwa katika muongozo wa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa yeye harudishi marashi wala hayakatai; kwasababu ni rahisi kubebeka na yana harufu nzuri, kama ilivyokuja katika riwaya nyingine.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kupendeza (ni sunna) kukubali zawadi ya marashi; kwasababu hayana gharama kuyabeba kwake wala haya masimango katika kuyakubali kwake.
  2. Ukamilifu wa tabia zake Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake katika kupenda kwake marashi na kutoyarudisha.
  3. Inapasa mtu atumie marashi siku zote, kwani hiyo ni alama ya uzuri wa mtu, vitu vizuri ni vya watu wazuri na vitu vibaya ni vya watu wabaya.