عن خولة الأنصارية رضي الله عنها قالت: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «إن رجالاً يَتَخَوَّضُون في مال الله بغير حق، فلهم النار يوم القيامة».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Khaula Al Answariy- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake-: "Hakika watu wanaovuruga katika mali ya Mwenyezi Mungu bila haki, watakuwa na adhabu ya moto siku ya kiyama".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Ameeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuhusu watu wanaofanya matumizi katika mali za waislamu kwa batili (bila ya haki), nakuwa wao wanazichukua bila haki, na inaingia katika hilo kula mali ya mayatima na mali ya wakfu (iliyotolewa sadaka) bila haki yake stahiki na kukanusha amana na kuzichukua bila haki stahiki wala idhini katika mali za umma, na akaeleza Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa malipo yao ni moto kwa hilo siku ya kiyama.