عن خولة الأنصارية رضي الله عنها قالت: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «إن رجالاً يَتَخَوَّضُون في مال الله بغير حق، فلهم النار يوم القيامة».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Khaula Al Answariy- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake-: "Hakika watu wanaovuruga katika mali ya Mwenyezi Mungu bila haki, watakuwa na adhabu ya moto siku ya kiyama".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuhusu watu wanaofanya matumizi katika mali za waislamu kwa batili (bila ya haki), nakuwa wao wanazichukua bila haki, na inaingia katika hilo kula mali ya mayatima na mali ya wakfu (iliyotolewa sadaka) bila haki yake stahiki na kukanusha amana na kuzichukua bila haki stahiki wala idhini katika mali za umma, na akaeleza Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa malipo yao ni moto kwa hilo siku ya kiyama.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ni haramu kwa mtu kuchuma mali ispokuwa kwa njia za halali, kwasababu kuzichuma kwa njia ya haramu ni kuzivuruga na ni kuzitumia vibaya.
  2. Mali iliyoko mkononi mwa waislamu na mkononi mwa viongozi hiyo ni mali ya Mwenyezi Mungu amewamilikisha juu yake ili waitumie katika njia ya kisheria, na kuitumia kwa batili ni haramu, na hili ni kwa viongozi wote na wengineo katika waislamu wote.