عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «إيَّاكم والظنَّ، فإن الظنَّ أكذبُ الحديث».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kutoka kwa Mtume rehema na Amani zimfikie, amesema: "Jiepusheni na dhana, kwani dhana ni maneno ya uongo".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Katika hadithi kuna tahadhari kutokana na dhana ambayo haijajengwa juu ya ushahidi, kiasi ambacho anaamini mtu juu ya dhana hii kavu isiyo na ushahidi na kisha anajenga hukumu juu yake, nakuwa hili ni katika tabia mbaya, nakuwa hili ni katika maneno ya uongo mno, kwasababu mdhaniaji atakapoyaamini yale yanayotegemewa na akayafanya kuwa ndiyo asili na akakata shauri kwayo tayari unakuwa ni uongo bali uongo mbaya mno.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Tahadhari kutokana na dhana ambayo haijajengeka juu ya ushahidi.
  2. Haidhuru dhana mbaya kwa mtu ambaye zimedhihiri kwake alama zake, kama watenda mabaya na maovu.
  3. Makusudio ni kutahadhari na tuhuma ambazo zinazokaa katika nafsi, na kuendelea nazo, ama yanayojitokeza katika nafsi wala hayakai haya mtu hachukuliwi dhambi kwayo.