عن أبي هريرة رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «الصلوات الخمس، والجمعة إلى الجمعة، ورمضان إلى رمضان مُكَفِّراتٌ لما بينهنَّ إذا اجتُنبَت الكبائر».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume rehema na Amani zimfikie, Amesema: "Swala tano, na Ijumaa mpaka Ijumaa, na ramadhani mpaka ramadhani vinafuta madhambi yaliyo kati yake, yatakapoepukwa madhambi makubwa".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Swala tano zinafuta yaliyo kati yake katika madhambi- nayo ni yale madogo- ispokuwa madhambi makubwa hakuna kinachoyafuta ispokuwa toba, na hivyo hivyo Ijumaa mpaka ijumaa inayofuata, na hivyo hivyo funga ya Ramadhani mpaka Ramadhani iliyo baada yake.