عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «لا تجعلوا بيوتكم قبورا، ولا تجعلوا قبري عيدا، وصلوا عليّ فإن صلاتكم تبلغني حيث كنتم».
[صحيح] - [رواه أبو داود]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani ziwe juu yake: "Msizifanye nyumba zenu kuwa makaburi, na wala msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, na mniombee rehema juu yangu, kwani maombi yenu hunifikia mahala popote mtakapokuwa".
Sahihi - Imepokelewa na Abuu Daud

Ufafanuzi

Amekataza rehema na Amani zimfikie kuziacha tupu nyumba kwa kutokuwa na swala za sunna ndani yake na dua na kusoma Qur'ani, zikawa ni kama makaburi, kwasababu katazo la kutoswalia makaburini limejirudia sana kwao, hivyo akawakataza wasizifanye nyumba zao kuwa hivyo, na amekataza kurudirudi katika ziara ya kaburi lake, na kukusanyika hapo kwa namna iliyozoeleka; kwasababu hilo ni njia inayopelekea katika ushirikina, na akaamrisha kutosheka na hilo kwa kukithirisha kumtakia rehema na Amani mahala popote katika ardhi; kwasababu sala hizo humfikia kutoka kwa aliyekaribu na wa mbali kwa kiwango sawa, hakuna haja ya kurudirudi katika kaburi lake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuharamishwa kuzihama nyumba kutokana na ibada za Mwenyezi Mungu.
  2. Kuziba njia zinazopelekea katika ushirikina, kuanzia katika kuswalia makaburini, na kuchupa mpaka katika kaburi lake rehema na Amani zimfikie, kwa kulifanya kuwa ni mahala pa kukusanyika na kufanya ziara maalumu za mara kwa mara.
  3. Kuzuiwa kusafiri kwaajili ya ziara ya kaburi lake rehema na Amani zimfikie.
  4. Kumuhami yeye rehema na Amani zimfikie upande wa Tauhidi.
  5. Nikuwa hakuna ubora wowote wakuwa karibu na kaburi lake rehema na Amani zimfikie.
  6. Sheria ya kumtakia rehema na Amani yeye katika pande zote za Ardhi.
  7. Uharamu wa kuswali makaburini.
  8. Uharamu wa kufanya ziara ya kaburi la Mtume rehema na Amani zimfikie kuwa sikukuu, kwa kurudi mara kwa mara kwa namna maalumu tena kwa wakati maalumu, na hivyo hivyo kulizuru kila kaburi.
  9. Kunufaika wafu kwa dua za waliohai.