عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «لا تجعلوا بيوتكم قبورا، ولا تجعلوا قبري عيدا، وصلوا عليّ فإن صلاتكم تبلغني حيث كنتم».
[صحيح] - [رواه أبو داود]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani ziwe juu yake: "Msizifanye nyumba zenu kuwa makaburi, na wala msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, na mniombee rehema juu yangu, kwani maombi yenu hunifikia mahala popote mtakapokuwa".
Sahihi - Imepokelewa na Abuu Daud
Amekataza rehema na Amani zimfikie kuziacha tupu nyumba kwa kutokuwa na swala za sunna ndani yake na dua na kusoma Qur'ani, zikawa ni kama makaburi, kwasababu katazo la kutoswalia makaburini limejirudia sana kwao, hivyo akawakataza wasizifanye nyumba zao kuwa hivyo, na amekataza kurudirudi katika ziara ya kaburi lake, na kukusanyika hapo kwa namna iliyozoeleka; kwasababu hilo ni njia inayopelekea katika ushirikina, na akaamrisha kutosheka na hilo kwa kukithirisha kumtakia rehema na Amani mahala popote katika ardhi; kwasababu sala hizo humfikia kutoka kwa aliyekaribu na wa mbali kwa kiwango sawa, hakuna haja ya kurudirudi katika kaburi lake.