عن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «كل معروف صدقة».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jabiri bin Abdillah Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Kila wema ni sadaka".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Kila wema anaoufanya mwanadamu ni sadaka, na sadaka ni kila anachokitoa mtoaji katika mali, na hii inakusanya sadaka za wajibu na za sunna, akabainisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa kufanya wema kuna hukumu ya sadaka katika malipo na thawabu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Hadithi inaonyesha kuwa sadaka haiishii katika yale aliyoyatoa mwanadamu katika mali zake, bali kila kitu anachokifanya mwanadamu au kukisema miongoni mwa kheri anaandikiwa kwake hicho kuwa ni sadaka.
  2. Hapa kuna kuhamasishwa katika kufanya mema na yote ambayo ndani yake yana manufaa kwa wengine.