عن عائشة رضي الله عنها مرفوعاً: «لا تسبوا الأموات؛ فإنهم قد أفضوا إلى ما قدموا».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, Hadithi Marfu'u: "Msiwatukane wafu: kwani wao tayari wameyaendea yale waliyoyatanguliza".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Hadithi hii ni dalili juu ya uharamu wa kuwatukana wafu na kujiingiza katika heshima zao, Nakuwa haya ni katika tabia mbaya, na hekima ya kukatazwa kwake imekuja katika kauli yake iliyobakia katika hadithi: "Kwani wao tayari wameyaendea yale waliyoyatanguliza" Yaani wameyafikia yale waliyoyatanguliza katika matendo yao mema au maovu, na matusi haya hayawafikii bali yanawaudhi waliohai.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Hadithi hii ni dalili juu ya uharamu wa kuwatukana wafu, na ujumla wake unaonyesha kuwa sawa sawa wao wawe ni waislamu au makafiri.
  2. Kunaondolewa katika swala la kuwatukana wafu, itakapokuwa kutaja aibu zao kuna faida.
  3. Hekima ya kukatazwa kuwatukana imekuja katika hadithi, nakuwa wao wameyafikia yale waliyoyatanguliza katika kheri au shari hivyo matusi hayawasaidii, Na yale yanayopatikana katika kuwaudhi waliohai.
  4. Nikuwa haifai kwa mtu kusema yale yasiyokuwa na faida.