عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال: سألت رسول الله صلى الله عليه وسلم أيُّ الذنب أعظم؟ قال: «أن تجعل لله نِدًّا، وهو خَلَقَكَ» قلت: ثم أَيُّ؟ قال: «ثم أن تقتل ولدك خَشْيَةَ أن يأكل معك» قلت: ثم أَيُّ؟ قال: «ثم أن تُزَانِي حَلِيْلَةَ جَارِكَ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdallah bin Masudi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Nilimuuliza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Ni dhambi ipi kubwa? Akasema: "Ni kumuwekea Mwenyezi Mungu mshirika, na haliyakuwa yeye ndiye aliyekuumba" Nikasema: kisha ipi? akasema: "Kisha kumuuwa mtoto wako ili asile pamoja nawe" Nikasema: kisha ipi? akasema: "Kisha na umzini mke wa jirani yako".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Waliuliza maswahaba Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao kuhusu madhambi makubwa akawaeleza kuhusu makubwa yake, nayo ni shirki kubwa, nayo ni ile ambayo haisamehe Mwenyezi Mungu Mtukufu ispokuwa kwa toba, na ikiwa atakufa mfanyaji wake basi huyo atakaa milele motoni. Kisha ni mtu kumuuwa mtoto wake kwa kuhofia kula naye, kuuwa nafsi ambayo ameiharamisha Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiyo daraja ya pili ya madhambi makubwa na yanazidi madhambi na adhabu inaongezeka akiwa aliyeuliwa ana udugu na muuwaji, na yanaongezeka mara nyingine pale inapokuwa sababu ya kuuwa ni kumkatisha aliyeuliwa na riziki ya Mwenyezi Mungu ambayo ameiweka mikononi mwa muuwaji. kisha akizini mtu na mke wa jirani yake, zinaa ndio daraja ya tatu ya madhambi makubwa, na yanakuwa makubwa madhambi atakapokuwa aliyeziniwa ni mke wa jirani ambaye sheria imeusia kumfanyia uzuri na wema na kuishi naye vizuri.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kutofautiana madhambi kwa ukubwa, kama yalivyo matendo mema yanatofautiana katika ubora.
  2. Hadithi inaonyesha juu ya madhambi makubwa: Kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu, kisha kuuwa nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameiharamisha ispokuwa kwa haki, kisha zinaa.