عَنِ أَبي عبدِ الرَّحمنِ عبدِ اللهِ بْنِ عُمَرَ بن الخَطَّابِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعتُ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: " بنِيَ الإِسْلاَمُ عَلَى خَمْسٍ: شَهَادَةِ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَأَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ، وَإِقَامِ الصَّلاَةِ، وَإِيتَاءِ الزَّكَاةِ، وَحَجِّ البَيتِ، وَصَوْمِ رَمَضَانَ".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Abdulrahman Abdillahi bin Omar bin Khattwab Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Akisema: "Umejengeka Uislamu juu ya mambo matano: kushuhudia kuwa hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na kuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na kusimamisha swala, na kutoa zaka, na kuhiji nyumba tukufu, na kufunga ramadhani".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Amepokea Abdallah bin Omar bin Khattwab Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao ya kwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: (Umejengwa uislamu juu ya mambo matano), Yaani: Uislamu mfano wake ni kama jengo, nakuwa mambo haya matano ndio yamekaa nafasi ya visaidizi na nguzo zake ambazo linapata uimara kwake; ya kwanza: ni kushuhudia kuwa hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yaani: Hakuna muabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na hili ndio neno la kumpwekesha Mwenyezi Mungu (Tauhidi) na haukubadili uislamu bila neno hilo, ni lazima kulitamka, na kujua maana yake, na kuyafanyia kazi malengo yake, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu; Na makusudio yake: Ni kumsadikisha katika yale yote aliyoyaeleza, katika yale ambayo yamethibiti upokezi wake kuwa yanatoka kwake, na kuyafanyia kazi yale aliyoyaamrisha,na kuyaepuka yale aliyoyakataza, nakuwa asiabudiwe Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa yale aliyoyafundisha kama sheria. Na ya pili: Kusimamisha swala, nayo ni nguzo muhimu mno baada ya shahada mbili, na hufanyika usiku na mchana mara tano, na ndio maana ni kiunganishi kizito kati ya mja na Mola wake, na kusimamisha swala: ni kuitekeleza katika namna ya kudumu. Na ya tatu: Ni kutoa zaka, Na zaka ni ibada ya mali hufanyika kwa mwaka mara moja, pale mwaka unapotimia, au wakati wa kupatikana matunda na kuiva kwake, na manufaa yake ni mapana, na ndio maana ikatangulizwa kabla ya Hija na swaumu, na ikafuata baada ya swala. Na ya nne: Ni kuhiji nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu, nayo ni ibada ya mwili; kwasababu mwanadamu anaifanya yeye mwenyewe, na inafaa kuwakilishwa pia kwa yule ambaye anastahiki kuwa badala yake, nayo pia ni ibada ya mali; kwani mtu anahitaji kuwa na mali, na akiba. Na ya tano: Ni kufunga ramadhani, na swaumu ni ibada ya mwili ila maslahi yake si mapana, bali ni kuyaacha baadhi ya mambo maalum kwa nia maalum, nayo ni yale yenye kufunguza, na swaumu ni wajibu katika mwaka mwezi mmoja, nao ni mwezi wa ramadhani. Na nguzo ya kwanza haukubaliki uislamu isipokuwa kwa nguzo hiyo, na ya pili ambayo ni swala pia hivyo hivyo, kutoka kwa Jaabir Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema: "Hakika kati ya mtu na kati ya ushirikina na ukafiri ni kuacha swala", Kaipokea Muslim, nayo inachukuliwa maana yake kama ilivyo dhahiri yake, na hakujathibi katika mlango huu wa swala hadithi inayopingana na hiyo, bali imekinzana na uchambuzi wenye kwenda kinyume kutokana na uelewa wa wema waliotangulia, na yamethibiti makubaliano ya maswahaba -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote- juu ya ukafiri wa mwenye kuiacha, Amesema Abdallah bin shakiki Al uqailiy: "Walikuwa maswahaba wa Muhammadi -Rehema na Amani ziwe juu yake- hawaoni katika matendo ambayo kuyaacha kwake ni ukafiri tofauti na swala". kaipokea Tirmidhiy katika kitabu chake Al Jaamii, na kaipokea Al Muruuziy katika mlango wa kutukuza heshima ya swala, na ama nguzo tatu zilizobakia atakayeziacha bila udhuru basi uislamu wake una mapungufu, naye atakuwa katika upotovu wa mbali, na atakuwa katika hatari kubwa, lakini hatokufuru kwa hilo; kwa kuonyeshwa hilo katika ushahidi mwingine.