Aina: Akida- Itikadi- .

عن عمر رضي الله عنه قال: «بينما نحن جلوسٌ عند رسول الله صلى الله عليه وسلم ذات يوم إذ طَلَعَ علينا رجلٌ شديد بياض الثياب، شديد سَواد الشعر، لا يُرى عليه أثرُ السفر ولا يعرفه منَّا أحدٌ، حتى جلس إلى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فأسنَد ركبتيْه إلى ركبتيْه، ووضع كفَّيه على فخذيْه، وقال: يا محمد أخبرْني عن الإسلام؟ فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : الإسلامُ أن تشهدَ أن لا إله إلا الله وأنَّ محمداً رسول الله، وتقيم الصلاة، وتُؤتيَ الزكاة، وتصومَ رمضان، وتحجَّ البيت إن استطعتَ إليه سبيلاً، قال: صدقتَ، فعَجِبْنا له يَسأله ويُصدِّقه، قال: فأخبرْني عن الإيمان؟ قال: أن تؤمنَ بالله وملائكته وكُتبه ورسُله واليوم الآخر، وتؤمن بالقدَر خيره وشرِّه، قال: صدقتَ، فأخبرْني عن الإحسان؟ قال: أن تعبدَ الله كأنَّك تراه، فإن لَم تكن تراه فإنَّه يراك، قال: فأخبرني عن الساعة؟ قال: ما المسؤول عنها بأعلمَ مِن السائل، قال: فأخبرني عن أمَاراتِها؟ قال: أنْ تلِدَ الأَمَةُ ربَّتَها، وأنْ تَرَى الحُفاةَ العُراة العَالَة رِعاءَ الشاءِ يَتَطاوَلون في البُنيان، ثمَّ انطلق فَلَبِثَ مليًّا ثم قال: يا عمر أتدري مَن السائل؟ قلتُ: الله ورسوله أعلم، قال: فإنَّه جبريلُ أتاكم يعلِّمُكم دينَكم».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Omar Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: "Tukiwa sisi tumekaa kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- siku moja, ghafla akatokeza mwanaume mmoja, mwenye nguo nyeupe sana, mwenye nywele nyeusi sana, hazionekani kwake athari za safari, na wala hakuna anayemfahamu yeyote katika sisi, mpaka akakaa kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akashijanisha magoti yake katika magoti mtume Rehema na Amani ziwe juu yake (mfano wa kikao cha tahiyatu) na akaweka mikono yake juu ya mapaja yake, Na akasema: Ewe Muhammadi, nieleze kuhusu Uislamu? Akasema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake: Uislamu ni kushuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu nakuwa Muhammadi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na usimamishe swala na utoe zaka, na ufunge Ramadhani, na uhiji nyumba tukufu ukipata uwezo wa kuifikia, Yule bwana akasema: "Swadakta"-Yaani: Umesema kweli, Tukamshangaa! Anamuuliza na anamsadikisha! Akasema: Nieleze kuhusu Imani? Akasema: Ni kumuamini Mwenyezi Mungu na Malaika wake na vitabu vyake na Mitume wake na siku ya mwisho, na uamini makadirio kheri yake na shari yake, Akasema: "Swadakta"-Yaani: Umesema kweli, Basi hebu nieleze kuhusu Ihsani (wema)? Akasema: Ni umuabudu Mwenyezi Mungu kana kwamba wewe unamuona, na ikiwa wewe humuoni basi yeye anakuona: Akasema: Hebu nieleze kuhusu kiyama: Akasema: hakuwa muulizwaji kuhusu hilo ni mjuzi kuliko muulizaji, Akasema: Hebu nieleze kuhusu dalili zake? Akasema: ni mjakazi kuzaa bwana yake, na ukawaona watembea peku na uchi na masikini wachunga mifugo wakishindana kujenga majengo marefu, kisha yule bwana akaondoka, akakaa muda kidogo kisha akasema: Ewe Omari unamjua ni nani huyo muulizaji? Nikasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wajuzi, Akasema: Basi bila shaka huyo ni Jibril alikuijieni ili akufundisheni dini yenu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Alijitokeza Jibrili -Amani iwe juu yake- kwa Maswahaba- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kwa sura ya mwanaume asiyefahamika, na wao wakiwa wamekaa kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, akakaa mbele ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, kikao cha mwenye kujifunza mwenye kutaka maelekezo, Akamuuliza kuhusu uislamu, akamjibu kwa nguzo hizi ambazo zinaambatana na kukiri shahada mbili, na kuhifadhi swala tano, na kutoa zaka kwa wastahiki wake, na kufunga mwezi wa ramadhani kwa nia ya kweli, na kutekeleza ulazima wa kuhiji kwa mwenye kuweza, akamsadikisha, wakashangaa maswahaba kwa swali lake linaloonyesha kutojua kwake kwa jinsi inavyoonekana, kisha kumsadikisha kwake yeye, na akamuuliza kuhusu imani na akamjibu kwa nguzo hizi sita, zinazoambatana nakuwa Mwenyezi Mungu ndiye muumbaji na mgawa riziki, anayesifika kwa ukamilifu aliyoepukana na mapungufu, nakuwa Malaika ambao amewaumba Mwenyezi Mungu ni waja waliyotukuzwa hawamuasi Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwa amri yake wanafanya, na kuamini vitabu vilivyoteremshwa kwa Mitume kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na Mitume wanaofikisha kutoka kwa Mwenyezi Mungu dini yake, nakuwa mwanadamu atafufuliwa baada ya kufa na atahesabiwa, kisha akamuuliza kuhusu wema (Ihsan) Akamueleza kuwa wema ni amuabudu Mwenyezi Mungu kana kwamba anamuona yeye Mtukufu, ikiwa kama hatoitekeleza ibada hii, basi amuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumuogopa yeye; kwa kujua kwake kuwa yeye anaona, na hakifichikani kwake chochote chenye kufichikana, kisha akabainisha kuwa ujuzi wa kiyama haujui yeyote katika viumbe, nakuwa katika dalili za kiyama ni kukithiri kwavijakazi na watoto wake, au kukithiri kwa uasi wa watoto kwa mama zao kiasi ambacho wanaishi nao kama wajakazi, nakuwa wachunga mbuzi na mafukara itafunguliwa kwao dunia zama za mwisho; watajifaharisha kwa kuyapamba majengo na kuyanyanyua juu, na maswali yote haya na majibu yake ni kwaajili ya kuifundisha dini hii tukufu kutoka kwa Jibrili kwa kauli ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake:"Huyu ni Jibrili alikujieni ili akufundisheni dini yenu".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuwekwa wazi Uzuri wa tabia za Mtume- Rehema na Amani ziwe juu yake- nakuwa yeye anakaa pamoja na maswahaba zake, na wao wanakaa kwake, na hajitengi akajiona kuwa yuko juu yao.
  2. Kupendezesha nguo na muonekano na usafi wakati wa kuingia kwa waheshimiwa, kwasababu Jibril alikuja kuwafundisha watu kwa hali (vitendo) na maneno.
  3. Nikuwa Malaika Amani iwe juu yao wanaweza kujibadilisha umbile lingine tofauti na umbile la kimalaika
  4. Kuwa mpole kwa muulizaji na kumsogeza, ili aweze kuuliza bila uoga wala hofu.
  5. Kuwa na adabu na mwalimu kama alivyofanya Jibrili Amani iwe juu yake, kiasi ambacho alikaa mbele ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kikao cha mwenye adabu ili aichukue elimu toka kwake.
  6. Kufaa kutaja jina la mtajwa bila kumuanisha, kwa ushahidi kauli yake aliposema: (Ewe Muhammadi) na ibara hii ni katika ibara zinazotumiwa na waarabu wa vijijini, akaacha kumuanisha kana kwamba ni mtu katoka kijijini, na kama si hivyo nikuwa watu wa mjini wenye kujipamba na tabia njema huwa hawamuiti Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kwa mfano kama huu.
  7. Kuwekwa wazi tofauti kati ya uislamu na imani na ihsan (wema).
  8. Nikuwa kuamini misingi sita ya imani ni katika jumla ya mambo ya kuamini ghaibu (yasiyoonekana).
  9. Nikuwa nguzo za Uislamu ni tano, nakuwa misingi ya imani ni sita.
  10. Nikuwa linapokutana neno uislamu na imani yanatafsirika uislamu kuwa ni yale mambo dhahiri, na imani kuwa ni yale mambo ya siri (ya ndani ya moyo).
  11. Kubainishwa utukufu wa daraja ya ihsan (wema).
  12. Nikuwa asili ya muulizaji ni kutokuwa na elimu, nakuwa ujinga ndio msukumo wa kuuliza.
  13. Kuanza na jambo la muhimu zaidi kisha la muhimu; kwasababu kumeanzwa na kutajwa shahada mbili katika kuufasiri uislamu, na kukaanzwa na kumuani Mwenyezi Mungu katika kuifasiri imani.
  14. Kuuliza kwa mjuzi katika yale asiyoyafahamu muulizaji, kwaajili ya kumfundisha msikilizaji.
  15. Kauli ya muulizwaji katika yale asiyoyajua: Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi.
  16. Nikuwa ujuzi wa kiyama ni miongoni mwa yale ambayo Mwenyezi Mungu elimu yake aliibakisha kwake.
  17. Kubainishwa sehemu katika alama za kiyama.