عن أبي ذر الغفاري رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم فيما يرويه عن ربه: «يا عبادي، إني حرَّمتُ الظلمَ على نفسي وجعلتُه بينكم محرَّمًا فلا تَظَالموا، يا عبادي، كلكم ضالٌّ إلا من هديتُه فاستهدوني أَهْدَكِم، يا عبادي، كلكم جائِعٌ إلا من أطعمته فاستطعموني أطعمكم، يا عبادي، كلكم عارٍ إلا من كسوتُه فاسْتَكْسُوني أَكْسُكُم، يا عبادي، إنكم تُخطئون بالليل والنهار وأنا أغفر الذنوبَ جميعًا فاستغفروني أغفرْ لكم، ياعبادي، إنكم لن تَبلغوا ضَرِّي فتَضُرُّونِي ولن تَبْلُغوا نَفْعِي فتَنْفَعُوني، يا عبادي، لو أن أولَكم وآخِرَكم وإنسَكم وجِنَّكم كانوا على أتْقَى قلبِ رجلٍ واحد منكم ما زاد ذلك في ملكي شيئًا، يا عبادي، لو أن أوَّلَكم وآخِرَكم وإنسَكم وجِنَّكم كانوا على أفْجَرِ قلب رجل واحد منكم ما نقص ذلك من ملكي شيئًا، يا عبادي، لو أن أولكم وآخركم وإنسكم وجنكم قاموا في صَعِيدٍ واحد فسألوني فأعطيت كلَّ واحدٍ مسألتَه ما نقص ذلك مما عندي إلا كما يَنْقُصُ المِخْيَطُ إذا أُدخل البحر، يا عبادي، إنما هي أعمالكم أُحْصِيها لكم ثم أُوَفِّيكُم إياها فمن وجد خيرًا فليحمد الله ومن وجد غير ذلك فلا يلومن إلا نفسه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Dhari Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika yale anayoyapokea kutoka kwa Mola wake: "Enyi waja wangu hakika Mimi nimeharamisha dhulma juu ya Nafsi yangu na nikaifanya kuwa ni haramu baina yenu, basi msidhulumiane, enyi waja wangu nyote ni wapotevu isipokuwa yule niliye muongoza, basi niombeni uongofu nami nitakuongozeni, enyi waja wangu nyote ni wenye njaa isipokuwa yule niliye mlisha, basi niombeni chakula nami nitakulisheni, enyi waja wangu nyote mpo uchi isipokuwa yule niliye mvisha, basi niombeni kuvishwa nami nitakuvisheni, enyi waja wangu hakika nyinyi mnakosea usiku na mchana na mimi ninasamehe madhambi yote, basi niombeni msamaha nami nitakusameheni, enyi waja wangu hamtafikia kufanya madhara mpaka mnidhuru wala hamtafanya mambo yenye manufaa mpaka mninufaishe, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakawa na ucha Mungu wa mtu mmoja hilo lisinge niongezea chochote katika Ufalme wangu, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakafanya uovu wa mtu mmoja hilo lisinge punguza chochote katika Ufalme wangu, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wangejikusanya katika uwanja mmoja wakaniomba nikampa kila mtu alicho kiomba hilo lisinge punguza chochote katika Ufalme wangu isipokuwa ni kama sindano inavyo punguza maji pindi inapo ingizwa baharini, enyi waja wangu si vinginevyo bali hakika matendo yenu yote nina wahifadhieni kisha nitawapa malipo yenu, mwenye kupata kheri amshukuru Mwenyezi Mungu, na atakayepata kinyume na hayo basi asimlamu yeyote isipokuwa nafsi yake) ((360)).
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Inatupa faida hadithi hii tukufu iliyokusanya faida kubwa katika misingi ya dini, na vipengele vyake, na adabu zake yakuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha dhulma juu ya nafsi yake kwa kujifadhilisha yeye, na wema kwa waja wake, na akaifanya dhulma kuwa ni haramu baina ya viumbe wake asimdhulumu yeyote mtu mwingine, nakuwa viumbe wote wamepotea katika njia ya haki isipokuwa kwa uongofu wa Mwenyezi Mungu na uwezo na taufiki yake, na atakayemuomba Mwenyezi Mungu basi atamuafikisha na atamuongoza, nakuwa viumbe ni mafakiri kwa Mwenyezi Mungu na ni wahitaji kwake, na atakayemuomba Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu atamkidhia haja zake na atamtosheleza, nakuwa wao wanafanya makosa usiku na mchana na Mwenyezi Mungu anayasitiri na anayaachilia mbali pale mja anapoomba msamaha, nakuwa wao hawawezi kwa vyovyote watakavyo jaribu kwa kauli zao na vitendo vyao kumdhuru Mwenyezi Mungu kwa chochote au kumnufaisha, nakuwa wao lau kama wangekuwa katika uchamungu wa moyo wa mtu mmoja au katika uovu wa moyo wa mtu mmoja, usingezidisha uchamungu wao katika ufalme wa Mwenyezi Mungu, wala usingepunguza uovu wao chochote katika ufalme wa Mwenyezi Mungu; kwasababu wao ni madhaifu tena mafukara kwa Mwenyezi Mungu na ni wahitaji kwake katika kila hali na nyakati na mahali, na kuwa wao lau wangesimama katika uwanja mmoja wakimuomba Mwenyezi Mungu akampa kila mmoja alichoomba, halitopunguza hilo yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu chochote; kwasababu hazina zake Mtukufu zimejaa hazipunguzwi na kutoa kokote, anamimina riziki usiku na mchana, nakuwa Mwenyezi Mungu anayahifadhi matendo ya waja na anayadhibiti yote mazuri yao na mabaya yao, kisha atawalipa kwayo siku ya kiyama, atakayekuta malipo ya matendo yake kuwa ni ya kheri basi na amshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumuafikisha kwake kumtii yeye, na atakayekuta malipo ya matendo yake chochote kinyume na hivyo, basi asimlaumu yeyote ila nafsi yake yenye kuamrisha maovu ambayo imemvuta mpaka katika hasara.