Aina: Akida- Itikadi- .

عن أبي ذر الغفاري رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم فيما يرويه عن ربه: «يا عبادي، إني حرَّمتُ الظلمَ على نفسي وجعلتُه بينكم محرَّمًا فلا تَظَالموا، يا عبادي، كلكم ضالٌّ إلا من هديتُه فاستهدوني أَهْدَكِم، يا عبادي، كلكم جائِعٌ إلا من أطعمته فاستطعموني أطعمكم، يا عبادي، كلكم عارٍ إلا من كسوتُه فاسْتَكْسُوني أَكْسُكُم، يا عبادي، إنكم تُخطئون بالليل والنهار وأنا أغفر الذنوبَ جميعًا فاستغفروني أغفرْ لكم، ياعبادي، إنكم لن تَبلغوا ضَرِّي فتَضُرُّونِي ولن تَبْلُغوا نَفْعِي فتَنْفَعُوني، يا عبادي، لو أن أولَكم وآخِرَكم وإنسَكم وجِنَّكم كانوا على أتْقَى قلبِ رجلٍ واحد منكم ما زاد ذلك في ملكي شيئًا، يا عبادي، لو أن أوَّلَكم وآخِرَكم وإنسَكم وجِنَّكم كانوا على أفْجَرِ قلب رجل واحد منكم ما نقص ذلك من ملكي شيئًا، يا عبادي، لو أن أولكم وآخركم وإنسكم وجنكم قاموا في صَعِيدٍ واحد فسألوني فأعطيت كلَّ واحدٍ مسألتَه ما نقص ذلك مما عندي إلا كما يَنْقُصُ المِخْيَطُ إذا أُدخل البحر، يا عبادي، إنما هي أعمالكم أُحْصِيها لكم ثم أُوَفِّيكُم إياها فمن وجد خيرًا فليحمد الله ومن وجد غير ذلك فلا يلومن إلا نفسه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Dhari Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika yale anayoyapokea kutoka kwa Mola wake: "Enyi waja wangu hakika Mimi nimeharamisha dhulma juu ya Nafsi yangu na nikaifanya kuwa ni haramu baina yenu, basi msidhulumiane, enyi waja wangu nyote ni wapotevu isipokuwa yule niliye muongoza, basi niombeni uongofu nami nitakuongozeni, enyi waja wangu nyote ni wenye njaa isipokuwa yule niliye mlisha, basi niombeni chakula nami nitakulisheni, enyi waja wangu nyote mpo uchi isipokuwa yule niliye mvisha, basi niombeni kuvishwa nami nitakuvisheni, enyi waja wangu hakika nyinyi mnakosea usiku na mchana na mimi ninasamehe madhambi yote, basi niombeni msamaha nami nitakusameheni, enyi waja wangu hamtafikia kufanya madhara mpaka mnidhuru wala hamtafanya mambo yenye manufaa mpaka mninufaishe, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakawa na ucha Mungu wa mtu mmoja hilo lisinge niongezea chochote katika Ufalme wangu, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakafanya uovu wa mtu mmoja hilo lisinge punguza chochote katika Ufalme wangu, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wangejikusanya katika uwanja mmoja wakaniomba nikampa kila mtu alicho kiomba hilo lisinge punguza chochote katika Ufalme wangu isipokuwa ni kama sindano inavyo punguza maji pindi inapo ingizwa baharini, enyi waja wangu si vinginevyo bali hakika matendo yenu yote nina wahifadhieni kisha nitawapa malipo yenu, mwenye kupata kheri amshukuru Mwenyezi Mungu, na atakayepata kinyume na hayo basi asimlamu yeyote isipokuwa nafsi yake) ((360)).
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Inatupa faida hadithi hii tukufu iliyokusanya faida kubwa katika misingi ya dini, na vipengele vyake, na adabu zake yakuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha dhulma juu ya nafsi yake kwa kujifadhilisha yeye, na wema kwa waja wake, na akaifanya dhulma kuwa ni haramu baina ya viumbe wake asimdhulumu yeyote mtu mwingine, nakuwa viumbe wote wamepotea katika njia ya haki isipokuwa kwa uongofu wa Mwenyezi Mungu na uwezo na taufiki yake, na atakayemuomba Mwenyezi Mungu basi atamuafikisha na atamuongoza, nakuwa viumbe ni mafakiri kwa Mwenyezi Mungu na ni wahitaji kwake, na atakayemuomba Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu atamkidhia haja zake na atamtosheleza, nakuwa wao wanafanya makosa usiku na mchana na Mwenyezi Mungu anayasitiri na anayaachilia mbali pale mja anapoomba msamaha, nakuwa wao hawawezi kwa vyovyote watakavyo jaribu kwa kauli zao na vitendo vyao kumdhuru Mwenyezi Mungu kwa chochote au kumnufaisha, nakuwa wao lau kama wangekuwa katika uchamungu wa moyo wa mtu mmoja au katika uovu wa moyo wa mtu mmoja, usingezidisha uchamungu wao katika ufalme wa Mwenyezi Mungu, wala usingepunguza uovu wao chochote katika ufalme wa Mwenyezi Mungu; kwasababu wao ni madhaifu tena mafukara kwa Mwenyezi Mungu na ni wahitaji kwake katika kila hali na nyakati na mahali, na kuwa wao lau wangesimama katika uwanja mmoja wakimuomba Mwenyezi Mungu akampa kila mmoja alichoomba, halitopunguza hilo yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu chochote; kwasababu hazina zake Mtukufu zimejaa hazipunguzwi na kutoa kokote, anamimina riziki usiku na mchana, nakuwa Mwenyezi Mungu anayahifadhi matendo ya waja na anayadhibiti yote mazuri yao na mabaya yao, kisha atawalipa kwayo siku ya kiyama, atakayekuta malipo ya matendo yake kuwa ni ya kheri basi na amshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumuafikisha kwake kumtii yeye, na atakayekuta malipo ya matendo yake chochote kinyume na hivyo, basi asimlaumu yeyote ila nafsi yake yenye kuamrisha maovu ambayo imemvuta mpaka katika hasara.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Katika maneno ya Mtume -sunna- yako ambayo ni maneno ya Mwenyezi Mungu, Nayo ni yale anayoyapokea Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kutoka kwa Mola wake, na huitwa kuwa ni Hadithil Qudsiy au Al-ilaahiy (Yaani: Hadithi Takatifu).
  2. Kuthibitisha kuzungumza kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu- nako ni kwingi katika Qur'ani Tukufu, nao ni ushahidi waliouzungumza Ahlus sunna (wenye kufuata mafundisho ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake) ya kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu yanakuwa kwa sauti, kwani hayaitwi maneno ispokuwa yale yenye kusikika.
  3. Mwenyezi Mungu Mtukufu anauwezo wa kudhulumu lakini yeye ameiharamisha dhulma juu ya nafsi yake kutokana na ukamilifu wa uadilifu wake.
  4. Uharamu wa dhulma.
  5. Sheria za Mwenyezi Mungu zimejengeka juu ya uadilifu.
  6. Miongoni mwa sifa za Mwenyezi Mungu ziko zilizo kanushwa mfano kama dhulma, lakini haipatikani katika sifa za Mwenyezi Mungu Mtukufu-sifa ya kukanusha pekee- ispokuwa kinapothibiti kinyume chake, kukanushwa dhulma kuna maanisha kuthibiti kwa uadilifu uliokamilika ambao hauna mapungufu ndani yake.
  7. Ana haki Mwenyezi Mungu Mtukufu ya kuharamisha juu ya nafsi yake ayatakayo kwasababu hukumu iko kwake, kama ambavyo anawajibisha juu ya nafsi yake ayatakayo.
  8. Kuiita nafsi kwa maana ya dhati kwa kauli yake: "Juu ya nafsi yangu" Na makusudio ya nafsi yake ni dhati yake -Aliyetakasika na kutukuka-.
  9. Ulazima wa kuelekea kwa Mola katika yote yanayomshukia mwanadamu, kwasababu ya kuhitajia viumbe vyote kwake.
  10. Ukamilifu wa uadilifu wa Mwenyezi Mungu na ufalme wake na utajiri wake na wema wake kwa waja wake, na ni juu ya waja waelekee kwa Mwenyezi Mungu katika kukidhi haja zao.
  11. Usitafute uongofu ispokuwa kwa Mwenyezi Mungu kwa kauli yake: "Niombeni uongofu nikuongozeni".
  12. Asili kwa watu wazima: ni kupotea, nako ni kutoijua haki na kuacha kuifanyia kazi.
  13. Yanayotokea kwa waja katika elimu au kuongoka, ni kwasababu ya uongofu wa Mwenyezi Mungu na mafundisho yake.
  14. Kheri yote ni katika fadhila za Mwenyezi Mungu kwa waja wake pasina kustahiki baadhi bila wengine, na shari yote inatoka kwa mwanadamu kwasababu ya kufuata matamanio ya nafsi yake.
  15. Nikuwa mwanadamu haumbi vitendo vya nafsi yake, bali yeye na vitendo vyake wote wameumbwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  16. Kwa vyovyote vile yatakavyokithiri madhambi na makosa hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu anayasamehe, lakini anahitaji mwanadamu aombe msamaha . na kwajili hiyo akasema: "Niombeni mimi msamaha nitakusameheni".
  17. Atakayefanya mema ni kwasababu ya msaada (taufiki) ya Mwenyezi Mungu na malipo yake ni fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu hivyo anastahiki sifa.