عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «إنَّ الله لا ينْظُرُ إِلى أجْسَامِكُمْ، ولا إِلى صُوَرِكمْ، وَلَكن ينْظُرُ إلى قُلُوبِكمْ وأعمالكم».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu hatazami katika mili yenu wala katika sura zenu, lakini anaangalia nyoyo zenu na matendo yenu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Hakika Mwenyezi Mungu hakupeni thawabu wala malipo kwa miili yenu na sura zenu wala haupatikani ukaribu kwake Mtukufu kwasababu ya hilo, lakini yanapatikana malipo kwasababu ya yale yaliyoko nyoyoni mwenu katika usafi wa nia (Ikhlaswi) na ukweli na kwa matendo mema mnayoyafanya.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kutilia umuhimu hali ya moyo na sifa yake, na kusahihisha dhamira zake, na kuzitwaharisha kutokana na kila sifa mbaya.
  2. Thawabu za matendo zinakuwa katika yale ambayo moyo umefungamana nayo miongoni mwa usafi wa nia (Ikhlaswi).
  3. kuzingatia sana kuurekebisha moyo na kwa sifa yake,na kuurekebisha moyo hilo linatangulia kwanza kabla ya matendo ya viungo, kwasababu matendo ya moyo ndio yanayosahihisha matendo ya kisheria, na halikubaliki jambo lolote kutoka kwa kafiri.
  4. Jukumu la kila mmoja juu ya nia yake na matendo yake, na haya ndiyo yanayompelekea kurekebisha matendo ya moyoni kwa kila linalomridhisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
Ziada