عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «إنَّ الله لا ينْظُرُ إِلى أجْسَامِكُمْ، ولا إِلى صُوَرِكمْ، وَلَكن ينْظُرُ إلى قُلُوبِكمْ وأعمالكم».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu hatazami katika mili yenu wala katika sura zenu, lakini anaangalia nyoyo zenu na matendo yenu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Hakika Mwenyezi Mungu hakupeni thawabu wala malipo kwa miili yenu na sura zenu wala haupatikani ukaribu kwake Mtukufu kwasababu ya hilo, lakini yanapatikana malipo kwasababu ya yale yaliyoko nyoyoni mwenu katika usafi wa nia (Ikhlaswi) na ukweli na kwa matendo mema mnayoyafanya.