عن عبادة بن الصامت رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم "مَنْ شهِد أنْ لا إله إلا الله وحده لا شرِيك له وأنَّ محمَّدا عبده ورسُولُه، وأنَّ عِيسى عبدُ الله ورسُولُه وكَلِمَتُه أَلقَاها إِلى مريم ورُوُحٌ مِنه، والجنَّة حَقٌّ والنَّار حقٌّ، أَدْخَلَه الله الجنَّة على ما كان مِنَ العمَل".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ubada bin swamit-Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume rehema na Amani zimfikie: "Atakaye shuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika nakuwa Muhammadi ni mjumbe wake na ni mja wake, nakuwa Issa ni mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na neno lake alilolipeleka kwa Mariam na ni roho toka kwake, na pepo ni kweli na moto ni kweli, Atamuingiza Mwenyezi Mungu peponi kulingana na yale aliyokuwa nayo katika matendo".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Inatueleza hadithi hii kuwa mwenye kutamka neno la Imani (Tauhiidi) na akajua maana yake na akayafanyia kazi malengo yake, na akashuhudia uja wa Muhammadi rehema na Amani zimfikie na ujumbe wake, na akakiri uja wa Issa na ujumbe wake, nakuwa yeye aliumbwa kwa neno "Kuwa" kutoka kwa Mariam, na akamuepusha mama yake na yale waliyomnasibishia maadui mayahudi, na akaitakidi kuthibiti kwa pepo kwa waumini na kuthibiti kwa moto kwa makafiri, na akafa katika imani hiyo ataingia peponi kulingana na yale yaliyokuwa katika matendo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa shahada mbili ndio msingi wa dini.
  2. Ubora wa tauhiidi nakuwa Mwenyezi Mungu anafuta kwayo makosa.
  3. Upana wa fadhila za Mwenyezi Mungu na wema wake- Aliyetakasika na kutukuka.
  4. Nikuwa itikadi ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu inapinga mila zote za kikafiri kutoka kwa mayahudi na wakristo, na waabudu masanamu na waabudu zama.(Nyakati)
  5. Hazikubaliki shahada mbili ispokuwa kwa yule aliyejua maana yake na akayafanyia kazi malengo yake.
  6. Amekusanya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Muhammadi rehema na Amani zimfikie kati ya uja na ujumbe, likiwa ni jibu kwa wanaopuuza na wanaovuka mipaka.
  7. Ulazima wa kuepuka kupuuza na kuvuka mpaka katika haki ya Manabii na watu wema, tusipinge ubora wao wala tusivuke mpaka tukawapatia kitu katika ibada, kama wanavyofanya baadhi ya wajinga na wapotofu.
  8. Kuthibitisha utumwa wa Issa na ujumbe wake, na hili ni jibu kwa wakristo waliodai kuwa yeye ni mwana wa Mungu.
  9. Nikuwa Isa ameumbwa kutoka kwa Mariam kwa neno "Kuwa" bila baba, na hili ni jibu kwa mayahudi waliomtuhumu Mariam kwa uzinifu.
  10. Nikuwa waovu katika wale waliompwekesha Mwenyezi Mungu hawatokaa milele motoni.
  11. Kuthibitisha sifa ya kuzungumza kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  12. Kuthibitisha kufufuliwa.
  13. Kuthibitisha pepo na moto.