عن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "مَنْ لَقِيَ الله لا يُشْرِك به شَيئا دخل الجنَّة، ومن لَقِيَه يُشرك به شيئا دخَل النار".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jaabir bin Abdillah radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Yakwamba Mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani zimfikie amesema: "Atakayekutana na Mwenyezi Mungu hali yakuwa hamshirikishi na chochote ataingia peponi, na atakaye kutananaye hali yakuwa anamshirikisha na chochote ataingia motoni".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anatueleza Mtume rehema na Amani zimfikie katika hadithi hii kuwa atakayekufa hali yakuwa hamshirikishi pamoja na Mwenyezi Mungu asiyekuwa yeye si katika uumbaji wala katika uungu wala katika majina na sifa ataingia peponi, na ikiwa atakufa katika hali ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu basi hakika makazi yake ni motoni.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Atakayekufa katika tauhidi hatokaa milele motoni na makazi yake ni peponi.
  2. Atakayekufa katika ushirikina utamuwajibikia kwake moto.
  3. Ukaribu wa pepo na moto kwa mja na kuwa hakuna kinachotenganisha kati yake na hivyo viwili ispokuwa kifo.
  4. Ulazima wa kuuogopa ushirikina; kwasababu kuokoka na moto kumewekewa sharti la kusalimika na ushirikina.
  5. Nikuwa si hoja wingi wa matendo, bali kinachozingatiwa ni kusalimika na ushirikina.
  6. Kubainishwa maana ya Laa ilaaha illa llaah- Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu- nayo kuacha ushirikina na kumpwekesha Mwenyezi Mungu kwa ibada.
  7. Ubora wa atakayesalimika na ushirikina.
  8. Kuthibitisha pepo na moto.
  9. Kinachozingatiwa katika matendo ni mwisho wake.