عن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول:
«مَنْ لَقِيَ اللهَ لَا يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا دَخَلَ الْجَنَّةَ، وَمَنْ لَقِيَهُ يُشْرِكُ بِهِ دَخَلَ النَّارَ».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 93]
المزيــد ...

Imepokelewa Kutoka kwa Jabiri bin Abdillah -Radhi za Allah ziwe juu yao- amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema:
"Atakayekutana na Mwenyezi Mungu akiwa hamshirikishi na chochote basi ataingia Peponi, na atakayekutana naye akimshirikisha ataingia Motoni".

[Sahihi] - [Imepokelewa Imamu Muslim] - [Swahiih Muslim - 93]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa mwenye kufa hali yakuwa hamshirikishi Mwenyezi Mungu na chochote basi mafikio yake ni katika Pepo hata kama ataadhibiwa kwa baadhi ya madhambi yake, nakuwa atakayekufa hali yakuwa anamshirikisha Mwenyezi Mungu na chochote atabakizwa milele Motoni.

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa tauhidi, nakuwa ni sababu ya kuokoka na kukaa milele Motoni.
  2. Ukaribu wa Pepo na Moto kwa mja nakuwa hakuna baina yake na hivyo viwili isipokuwa kifo.
  3. Tahadhari inatolewa ya kujiepusha na ushirikina mdogo au mkubwa, kwa sababu kuokoka na moto ni kwa kuuepuka.
  4. Mazingatio katika matendo huangaliwa mwisho wake.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (67)