عن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "مَنْ لَقِيَ الله لا يُشْرِك به شَيئا دخل الجنَّة، ومن لَقِيَه يُشرك به شيئا دخَل النار".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Jaabir bin Abdillah radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Yakwamba Mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani zimfikie amesema: "Atakayekutana na Mwenyezi Mungu hali yakuwa hamshirikishi na chochote ataingia peponi, na atakaye kutananaye hali yakuwa anamshirikisha na chochote ataingia motoni".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Anatueleza Mtume rehema na Amani zimfikie katika hadithi hii kuwa atakayekufa hali yakuwa hamshirikishi pamoja na Mwenyezi Mungu asiyekuwa yeye si katika uumbaji wala katika uungu wala katika majina na sifa ataingia peponi, na ikiwa atakufa katika hali ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu basi hakika makazi yake ni motoni.