عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "مَنْ مات وهو يدعُو مِنْ دون الله نِدًّا دخَل النَّار".
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillah bin Masudi -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani zimfikie amesema: "Atakayekufa naye akiomba kinyume na Mwenyezi Mungu mshirika, ataingia motoni".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Anatueleza Mtume rehema na Amani zimfikie katika hadithi hii kuwa yeyote atakayebadilisha chochote katika vile ambavyo ni maalumu kwa Mwenyezi Mungu kwa asiyekuwa yeye, na akafa akiwa katika hali hiyo, basi hakika makazi yake ni katika moto.