عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "مَنْ مات وهو يدعُو مِنْ دون الله نِدًّا دخَل النَّار".
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillah bin Masudi -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani zimfikie amesema: "Atakayekufa naye akiomba kinyume na Mwenyezi Mungu mshirika, ataingia motoni".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Anatueleza Mtume rehema na Amani zimfikie katika hadithi hii kuwa yeyote atakayebadilisha chochote katika vile ambavyo ni maalumu kwa Mwenyezi Mungu kwa asiyekuwa yeye, na akafa akiwa katika hali hiyo, basi hakika makazi yake ni katika moto.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Atakayefia katika ushirikina ataingia motoni, ikiwa ni shirki kubwa atawekwa milele motoni, na ikiwa ni shirki ndogo basi ataadhibiwa kwa kadiri atakavyotaka Mwenyezi Mungu kumuadhibu kisha atatolewa.
  2. Hakika kinachozingatiwa katika matendo ni mwisho wake.
  3. Nikuwa dua ni ibada haipelekwi ispokuwa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Ziada