Aina ndogo

Orodha ya Hadithi

Laana za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mayahudi na Wakristo, waliyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa misikiti- Anatahadharisha waliyoyafanya- na lau isingekuwa kauli hiyo basi lingedhihirishwa kaburi lake, (Angezikwa nje) ispokuwa alihofia kufanywa kuwa msikiti.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mimi nimejitosheleza na washirika juu ya kushirikishwa; atakayefanya jambo lolote akamshirikisha pamoja nami mwingine nitamuacha na shirki yake au (na mshirika wake).
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mimi najiepusha kwa Mwenyezi Mungu kuwa kwangu kati yenu na rafiki wa ndani, kwani Mwenyezi Mungu amenifanya mimi kuwa kipenzi wa ndani kama alivyomfanya Ibrahim kuwa kipenzi wa ndani, na lau kama ningejifanyia kipenzi wa ndani katika umma wangu basi ningemfanya Abuubakari kuwa kipenzi wa ndani.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
"Msichupe mipaka katika kunisifu kama walivyochupa mipaka manaswara kwa mwana wa Mariam, bila shaka hakika mimi ni mja wake, basi semeni; mja wa Mwenyezi Mungu na mjumbe wake"
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ni nani atakayefurahika zaidi kwa utetezi wako? Akasema: Atakayesema Laa ilaaha illa llaahu (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu) kwa nia safi toka moyoni mwake.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayekufa naye akiomba kinyume na Mwenyezi Mungu mshirika, ataingia motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Wameangamia wenye kujilazimisha -Alilisema hilo mara tatu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Je nikuagize katika yale aliyoniagiza kwayo Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake? Usiache picha yoyote ispokuwa umeifuta, wala kaburi lililonyanyuliwa ispokuwa umelisawazisha.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Madhambi makubwa kuliko yote: Ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu, na kujiaminisha na adhabu za Mwenyezi Mungu, na kukata tamaa na rehema za Mwenyezi Mungu, Na kufa moyo katika huruma za Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba yeye alikuwa pamoja na Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake katika baadhi ya safari zake, akatuma mjumbe asibakishe katika shingo ya mnyama chochote kinachotundikwa ispokuwa kikatwe.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenye kukitegemea kitu hufungamanishwa kwacho
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayesema: Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, na akayapinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu, ni haramu mali yake, na damu yake, na hesabu yake ni juu ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Malaika huteremka katika mawingu- wakalitaja jambo lililopitishwa mbinguni, basi shetani huiba kusikia, na akalisikia, kisha akaliteremsha kwa makuhani kisha wanaongopa pamoja na neno hilo uongo mia moja toka kwao wenyewe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msiswali makaburini, wala msiyakalie makaburi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hao ni watu ambao anapokufa kwao mja mwema, au mtu mwema, wanajenga juu ya kaburi lake msikiti, na wanachora hapo mapicha, hao ni viumbe waovu mbele ya Mwenyezi Mungu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Basi tambua kuwa haki za Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni wamuabudu yeye na wala wasimshirikishe na kitu chochote, na haki za waja kwa Mwenyezi Mungu asimwaadhibu yeyote ambaye hajamshirikisha yeye na chochote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakaye kufa hali ya kuwa hamshirikishi Mwenyezi Mungu na kitu chochote ataingia peponi, na atakaye kufa akiwa anamshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu chochote ataingia motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni msije kuapa (kupitia) kwa baba zenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Msiseme: Ni matakwa ya Mwenyezi Mungu na matakwa ya fulani, lakini semeni: Ni matakwa ya Mwenyezi Mungu kisha akataka fulani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
kuapa kwangu kwa jina la Mwenyezi Mungu kwa uongo napenda zaidi kuliko kuapa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu nikisema ukweli
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakuna kuambukizana maradhi, wala kutuhumu mikosi kwa sababu ya ndege, na kinachonipendeza zaidi ni kujipa matumaini. Wakasema: Ni nini matumaini? Akasema: Ni neno jema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Tulikuwa kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- watu tisa au nane au saba, akasema: Hivi hamumpi ahadi ya utiifu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayepatwa na umasikini akaushusha kwa watu hautozibwa umasikini wake, na atakayeushusha kwa Mwenyezi Mungu, basi ni karibu zaidi Mwenyezi Mungu kumpa riziki ya haraka au ya baadaye
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake mtafuata nyenendo za wale waliokuwa kabla yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba mtu mmoja alikuja kwa Mtume rehema na amani zimfikie, akamsemesha katika baadhi ya mambo, akasema: Akitaka Mwenyezi Mungu na ukataka, akasema Mtume rehema na amani zimfikie: "Umenifanya mimi kuwa mshirika wa Mwenyezi Mungu? sema: Akitaka Mwenyezi Mungu pekee
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayetundika hirizi atakuwa kafanya ushirikina
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa