+ -

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رضي الله عنه عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«لَا عَدْوَى، وَلَا طِيَرَةَ، وَيُعْجِبُنِي الْفَأْلُ» قَالَ قِيلَ: وَمَا الْفَأْلُ؟ قَالَ: «الْكَلِمَةُ الطَّيِّبَةُ».

[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anasi Bin Maliki -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Hakuna kuambukizana maradhi, wala kutuhumu mikosi kwa sababu ya ndege, na kinachonipendeza zaidi ni kujipa matumaini". Wakasema: Ni nini matumaini? Akasema: "Ni neno jema".

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa kuambukizana ambako walikuwa wakiamini watu wa zama za ujinga kuwa maradhi yanahama yenyewe kwenda kwa mwingine pasina kadari ya Mwenyezi Mungu, nikuwa madai hayo ni batili, nakuwa mikosi ya ndege ni batili, nayo ni mikosi kupitia kitu chochote chenye kuhisika au kuonekana, kama ndege au wanyama, au walemavu, au namba au siku au kinginecho, hapa ametaja ndege kwa sababu ni kitendo kilichokuwa maarufu zama za ujinga, na asili yake ilikuwa ni kumuachia ndege wakati wa kuanza kazi yoyote, kama safari au biashara au kinginecho, akiruka kuelekea kushoto mtu anaamini ni mkosi, na anaahirisha alichotaka kukifanya. Kisha akaeleza -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa anafurahishwa sana na mtu kujipa matumaini, nayo ni mtu kuwa na furaha na raha, kwa maneno mazuri anayoyasikia, yatakayomfanya awe na dhana nzuri na Mola wake Mlezi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الغوجاراتية اليوروبا الدرية الصومالية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kumtegemea Mwenyezi Mungu Mtukufu, nakuwa hakuna awezaye kuleta kheri isipokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna awezaye kuzia shari isipokuwa Mwenyezi Mungu.
  2. Katazo la kuamini mikosi ya ndege, nayo ni kila kitu kinachoaminika kuwa ni mkosi, na kufanya kazi isifanyike.
  3. Matumaini si katika mikosi iliyokatazwa, bali ni katika kumdhania kheri Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  4. Kila kitu kinachotokea ni kwa mipango na makadirio ya Mwenyezi Mungu Mtukufu peke yake, yeye pekee asiye na mshirika wake.
Ziada