عن زيد بن خالد الجهني رضي الله عنه مرفوعاً: «مَنْ جَهَّز غَازِياً فِي سَبِيلِ الله فَقَد غَزَا، وَمَنْ خَلَّف غَازِياً في أهلِه بخَير فقَد غزَا».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa zaidi bin Harith Al-juhaniy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakayemuandaa mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu basi na yeye atakuwa kapigana, na atakayemsimamia mpiganaji katika familia yake basi na yeye atakuwa kapigana".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Mtu Atakapomuandaa mpiganaji kwa kipandwa chake na bidhaa zake na silaha zake, Mwenyezi Mungu anamuandikia malipo ya mpiganaji; kwasababu yeye kamsaidia katika kheri, na lau kama mpiganaji akitaka kupigana lakini familia yake ikampa uzito ni nani atakayewasimamia wanapokuwa na haja, akamuita mtu miongoni mwa waislamu na akasema: Niangalizie familia yangu kwa kheri, basi huyu aliyemuacha naye anakuwa na malipo ya mpiganaji; kwasababu kamsaidia, na inachukuliwa katika hili kuwa yeyote mwenye kumsaidia mtu katika jambo la kumtii Mwenyezi Mungu basi atapata malipo sawa na malipo yake, anaposaidiwa mwanafunzi katika kununuliwa vitabu, au kulipiwa kodi ya nyumba, au matumizi, au mfano wa hayo, basi atakuwa na malipo mfano wa malipo yake, bila kupungua katika malipo yake chochote.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama