عن أبي عَبْس عبد الرحمن بن جبر رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «ما اغْبَرَّتْ قَدَمَا عَبْدٍ في سَبِيل الله فَتَمَسَّهُ النَّار».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Absi Abdir-Rahmani bin Jabri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Haijawahi kupata vumbi miguu ya mja yeyote katika njia ya Mwenyezi Mungu, halafu ikaguswa na moto".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Maana ya hadithi: nikuwa yule anayetoka barabarani kwaajili ya kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu -Mtukufu- ikapata vumbi miguu yake hiyo itakuwa ni sababu ya kumkinga na moto, na katika tamko la Bukhariy: "Itakayepata vumbi miguu yake katika njia ya Mwenyezi Mungu atamharamisha Mwenyezi Mungu na moto".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama