عن عبدالله بن عباس رضي الله عنهما أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «ما من أيام العمل الصالح فيها أحب إلى الله من هذه الأيام» يعني أيام العشر. قالوا: يا رسول الله، ولا الجهاد في سبيل الله؟ قال: «ولا الجهاد في سبيل الله، إلا رجل خرج بنفسه وماله، فلم يَرْجِعْ من ذلك بشيء»
[صحيح] - [رواه البخاري، وهذا لفظ أبي داود وغيره]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillahi bin Abbasi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Hakuna siku ambazo matendo mema yanapendeka zaidi ndani yake kwa Mwenyezi Mungu kama masiku haya". Yaani masiku kumi. wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hata jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Akasema: "Hata jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, ispokuwa mtu aliyetoka kwa nafsi yake na mali yake, na kikawa hakikurudi chochote katika hivyo".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
"Hakuna siku ambazo matendo mema yanapendeka zaidi ndani yake kwa Mwenyezi Mungu kama masiku haya". Yaani masiku kumi. wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hata jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Akasema: "Hata jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, ispokuwa mtu aliyetoka kwa nafsi yake na mali yake, na kikawa hakikurudi chochote katika hivyo" kauli yake: "Matendo mema" Inakusanya swala na sadaka na swaumu na dhikiri na kumtukuza Mwenyezi Mungu na kusoma Qur'ani na wema kwa wazazi wawili, na kuunga udugu na kuwafanyia wema viumbe, na kuwa na ujirani mwema, na mengineyo katika matendo mema, hivyo ni sunna kufunga siku kumi za mwanzo wa Dhil-Hijja kwa kuingia kwake katika ujumla wa matendo mema, na makusudio yake kasoro siku ya kumi; kwasababu ya katazo la kufunga siku ya Idd. Na katika hili kuna ubora wa matendo mema katika siku kumi za mwanzo katika mwezi wa Dhul-Hijja, na kuna dalili pia kuwa Jihadi ni katika matendo bora, na ndio maana alisema swahaba: "Hata kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu", na kuna dalili juu ya hali hizi chache kuwa; atoke mtu kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa nafsi yake na mali yake- na mali yake yaani: silaha yake na kipandwa chake- kisha anauawa na inachukuliwa silaha yake na kipandwa chake kinachukuliwa na adui, Huyu kapoteza nafsi yake na mali yake katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi yeye ni katika wapiganaji bora, na huyu ndiye mbora zaidi kuliko matendo mema ndani ya siku kumi za mwezi Dhul-Hijja, na likifanyika jambo hili ndani ya siku kumi basi unaongezeka ubora wake.