عن البراء بن عازب رضي الله عنهما أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم قال في الأَنصَار: «لاَ يُحِبُّهُم إِلاَّ مُؤمِن، وَلاَ يُبْغِضُهُم إِلاَّ مُنَافِق، مَنْ أَحَبَّهُم أَحَبَّهُ الله، وَمَنْ أَبْغَضَهُم أَبْغَضَه اللَّه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Barraa bin A'zib -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alisema kuhusu maanswari (waliowapokea maswahaba waliohama kutoka Makka): "Hawapendi mtu ila muumini,na hawachukii ila mnafiki, atakayewapenda Answaar na Mwenyezi Mungu atampenda,na atakayewachukia Mwenyezi Mungu atamchukia".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Ameeleza Barraa bin A'zib -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alihimiza juu ya kuwapenda maanswari, na akalifanya hilo kuwa ni alama ya imani; kwa kutimiza mazuri waliyoyafanya maanswari; na hii ni kwasababu ya kutangulia kwao kuuhudumia ujumbe wa mtume, na yale waliyoyafanya ya kuinusuru dini ya uislamu, na kufanya haraka kuidhihirisha na kuwapa hifadhi waislamu, na kusimamia kwao juu ya majukumu ya uislamu ukweli wa kusimamia, na kumpenda kwao Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- nakuwapenda kwake wao, na kuzitoa kwao mali zao mbele yake, na kupigana kwao na kuwafanyia kwao uadui watu wengine kwa kuipa kipaumbele dini ya uislamu, bali ameweka wazi mkweli mwenye kusadikishwa kuwa hakika kuwachukia hakutarajiwi ila kwa mtu mnafiki asiyemuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho aliyezamia katika unafiki.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama