عن حفصة بنت عمر بن الخطاب رضي الله عنهما عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: "من أتَى عرَّافًا فسأله عن شيء، فصدَّقه لم تُقْبَلْ له صلاةٌ أربعينَ يومًا".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Hafswa bint Omari bin Khattwabi- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayemuendea mpiga ramli akamuuliza kuhusu lolote, akamsadikisha, haitokubaliwa kwake swala yoyote siku arobaini".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anatueleza Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii kuwa; yeyote atakayekuja kwa mpiga ramli miongoni mwa wapiga ramli- Naye ni yule anaye dai kujua mambo yaliyofichikana- akamuuliza kuhusu kitu miongoni mwa mambo yaliyofichikana, na akamsadikisha kwa yale anayoyasema, basi hakika Mwenyezi Mungu atamnyima katika thawabu za swala yake siku arobaini, na hiyo ni adhabu kwake juu ya yale aliyoyaendea katika makosa na madhambi makubwa, ama atakayewasadikisha atakuwa kakufuru yale yaliyoteremshwa kwa Muhammadi Rehema na Amani ziwe juu yake, kama ilivyokuja katika hadithi nyingine, na ikiwa haya ndiyo malipo ya mwenye kumuendea kuhani, basi je? yakoje malipo ya kuhani mwenyewe! Tunajilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na hilo na tunamuomba Mwenyezi Mungu atupe afya.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Katazo la kwenda kwa makuhani na kuwauliza kuhusu mambo yaliyofichikana na kuwasadikisha katika hilo, nakuwa hilo ni ukafiri.
  2. Uharamu wa ukuhani, nakuwa hilo ni katika madhambi makubwa.
  3. Anaweza kunyimwa mwanadamu thawabu za utiifu, kama adhabu kwake kwa kufanya kwake maasi.