عن ابن عباس رضي الله عنهما قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : "من اقتَبَس شُعْبَة من النُّجوم؛ فقد اقتَبَسَ شُعْبة من السِّحْر، زاد ما زاد".
[صحيح] - [رواه أبو داود وابن ماجه وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Ibn Abbasi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu- Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Atakayejifunza sehemu katika elimu ya nyota; basi atakuwa kajifunza sehemu katika uchawi, amezidisha anavyozidisha". Yaani: kila anavyozidi kujifunza ndivyo anavyozidisha uchawi.
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah
Na kwakuwa ilivyo, ghaibu ni katika mambo ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu- ameyabakisha kwake- Amebatilisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- kila jaribio la kutaka kubaini na kuchungulia katika siri zake, na miongoni mwa hayo ni elimu ya nyota- Ambayo ni kutoa ushahidi kupitia hali ya anga juu ya matukio ya ardhini, amebainisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa kujifunza hili ni aina ya uchawi, nakuwa kila anavyozidisha mtu jambo basi anakuwa kazidisha uchawi.