عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه مرفوعاً: «إن الله ليُمْلِي للظالم، فإذا أخذه لم يُفْلِتْهُ»، ثم قرأ: (وكذلك أخذ ربك إذا أخذ القرى وهي ظالمة إن أخذه أليم شديد).
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Musa Al-Ash'ariy Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu humpa muda mtu dhalimu, basi anapomshika hamuachii", kisha akasoma: "Na hivyo ndivyo anavyoadhibu Mola wako, anapokiadhibu kijiji kikiwa kimedhulumu, hakika kuadhibu kwake ni kwenye kuumiza na ni kukali".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Anaeleza Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka humpa muda mtu dhalimu na anamuacha aendelee kuidhulumu nafsi yake, mpaka anapomuadhibu hamuachi mpaka amkamilishie adhabu yake, kisha akasoma: "Na hivyo ndivyo anavyoadhibu Mola wako, anapokiadhibu kijiji kikiwa kimedhulumu, hakika kuadhibu kwake ni kwenye kuumiza na ni kukali".