Aina: Akida- Itikadi- .

عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه مرفوعاً: «إن الله ليُمْلِي للظالم، فإذا أخذه لم يُفْلِتْهُ»، ثم قرأ: (وكذلك أخذ ربك إذا أخذ القرى وهي ظالمة إن أخذه أليم شديد).
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Musa Al-Ash'ariy Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu humpa muda mtu dhalimu, basi anapomshika hamuachii", kisha akasoma: "Na hivyo ndivyo anavyoadhibu Mola wako, anapokiadhibu kijiji kikiwa kimedhulumu, hakika kuadhibu kwake ni kwenye kuumiza na ni kukali".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka humpa muda mtu dhalimu na anamuacha aendelee kuidhulumu nafsi yake, mpaka anapomuadhibu hamuachi mpaka amkamilishie adhabu yake, kisha akasoma: "Na hivyo ndivyo anavyoadhibu Mola wako, anapokiadhibu kijiji kikiwa kimedhulumu, hakika kuadhibu kwake ni kwenye kuumiza na ni kukali".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Mwenye akili hajiaminishi na adhabu za Mwenyezi Mungu anapodhulumu na akawa hajapatwa na udhia bali anajua kuwa hilo ni kupewa muhula, hivyo hufanya haraka kurudisha haki kwa watu wake.
  2. Huwapa muhula Mwenyezi Mungu watu madhalimu ili wazidishe madhambi, ili wazidishiwe adhabu.
  3. Maneno bora yanayofasiri hadithi au Qur'ani ni maneno ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake.