عن أبي هريرة رضي الله عنه : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «ينزلُ ربُّنا تبارك وتعالى كلَّ ليلةٍ إلى السماء الدنيا، حين يبقى ثُلُثُ الليل الآخرُ يقول: «مَن يَدْعُوني، فأستجيبَ له؟ مَن يسألني فأعطيَه؟ مَن يستغفرني فأغفرَ له؟».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Huteremka Mola wetu Aliyetakasika na kutukuka kila usiku katika mbingu ya dunia pindi inapobakia theluthi ya mwisho ya usiku, Anasema: "Nani mwenye kuniita, nimjibu, nani mwenye kuniomba nimpe, nani mwenye kuniomba msamaha nimsamehe".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Huteremka Mola wetu -Aliyetakasika na kutukuka- kila usiku katika theluthi ya mwisho katika mbingu ya dunia, kisha Anasema: "Nani mwenye kuniita, nimjibu, nani mwenye kuniomba nimpe, nani mwenye kuniomba msamaha nimsamehe" Yaani: yeye Mtukufu katika wakati huu wa usiku- Anataka kutoka kwa waja wake wamuombe, na anawahamasisha katika hilo, hivyo yeye anamjibu mwenye kumuita, na anawataka wamuombe wanayoyataka, hivyo yeye anampa mwenye kumuomba, na anataka toka kwao wamuombe msamaha kutokana na makosa yao, hivyo yeye huwasamehe waja wake waumini, na makusudio ya kuwataka; ni kuhimiza na kuita. Na kushuka huku ni kushuka kwa uhakika, kunakoendana na utukufu wake na ukamilifu wake, hakufanani na kushuka kwa viumbe, na wala haikubaliki kupindisha neno kushuka kuwa zinashuka rehema au Malaika, bali ni wajibu kuamini kuwa Mwenyezi Mungu anateremka mpaka mbingu ya dunia kuteremka kunakoendana na utukufu wake, bila kupindisha wala kubadili, na bila kuuliza uliza wala kufananisha, kama jinsi ulivyo msimamo wa Ahlus sunna wal Jama'a (wenye kumfuata Mtume na wema waliotangulia).