عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الخُدْرِيَّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ -وَكَانَ غَزَا مَعَ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ثِنْتَيْ عَشْرَةَ غَزْوَةً- قَالَ: سَمِعْتُ أَرْبَعًا مِنَ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَأَعْجَبْنَنِي، قَالَ:
«لاَ تُسَافِرِ المَرْأَةُ مَسِيرَةَ يَوْمَيْنِ إِلَّا وَمَعَهَا زَوْجُهَا أَوْ ذُو مَحْرَمٍ، وَلاَ صَوْمَ فِي يَوْمَيْنِ: الفِطْرِ وَالأَضْحَى، وَلاَ صَلاَةَ بَعْدَ الصُّبْحِ حَتَّى تَطْلُعَ الشَّمْسُ، وَلاَ بَعْدَ العَصْرِ حَتَّى تَغْرُبَ، وَلاَ تُشَدُّ الرِّحَالُ إِلَّا إِلَى ثَلاَثَةِ مَسَاجِدَ: مَسْجِدِ الحَرَامِ، وَمَسْجِدِ الأَقْصَى، وَمَسْجِدِي هَذَا».

[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Saidi Al-Khudri radhi za Allah ziwe juu yake na alikuwa kapigana vita pamoja na Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- takriban vita kumi na mbili (12) anasema: Nilisikia mambo manne kutoka Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, yakanifurahisha sana, anasema:
"Asisafiri mwanamke mwendo wa siku mbili mpaka awe pamoja na mume wake, au maharimu yake (Ndugu asiyeweza kumuoa), hakuna kufunga ndani ya siku mbili: Idil Fitri na Idil Adh-ha, na hakuna swala baada swala ya Asubuhi mpaka lichomoze jua, na wala baada ya Lasiri mpaka lizame, na wala haifungwi safari isipokuwa katika misikiti mitatu: Msikiti mtukufu (wa Makka), na Msikiti wa Aqswa (Palestina), na msikiti wangu huu (Madina)".

Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Amekataza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mambo manne:
La kwanza: Kamkataza mwanamke kusafiri mwendo wa siku mbili bila kuwa na mume wake au mmoja kati ya maharimu wake, naye ni mtu aliyeharamu kwake kumuoa uharamu wa moja kwa moja (usio wa moja kwa moja, kama mume wa dada yake) kama mwanaye, na baba, na mtoto wa kaka, na kijana wa dada, na baba mdogo au mkubwa, na mjomba, na mfano wake.
La pili: Katazo la kufunga siku Idil Fitri na siku ya Idil Adh-ha, sawa sawa muislamu amezifunga kwa udhuru au kwa kujitolea, au kafara.
La tatu: Amekataza kusali swala ya sunna baada ya swala ya Lasiri mpaka lizame Jua, na baada ya kuchomoza asubuhi mpaka lichomoze Jua.
La nne: Katazo la kusafiri kwenda eneo katika maeneo kwa itikadi kuwa kuna ubora, na kuitakidi kuwa kuna kulipwa malipo mengi, isipokuwa misikiti hii mitatu, hivyo hakuna kufunga safari kwenda misikiti isiyokuwa hiyo kwa ajili kuswali ndani yake, kwani malipo hayalipwi kwa wingi isipokuwa katika misikiti hii mitatu, Msikiti mtukufu (wa Makka), na Msikiti wa Mtume (Madina), na Msikiti wa Aqswa (Palestina).

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Haifai kwa mwanamke kusafiri bila maharim.
  2. Mwanamke hawezi kuwa maharim wa mwanamke mwenzie katika safari; kwa kauli yake: "Mume wake, au aliyeharamu kwake kumuoa (Maharim)"
  3. Kila inayoitwa safari basi mwanamke anakatazwa kusafiri bila mume wake au maharim yake, na hadithi ilikuwa kulinga na hali ya muulizaji na mji wake.
  4. Maharim wa mwanamke ni mume wake au aliyeharamu kwake kumuoa kwa uharamu wa moja kwa moja, kwa sababu ya udugu wa damu, kama baba na mtoto na baba mdogo au mkubwa na mjomba, au kwa kunyonya, kama baba wa kunyonya au baba mdogo wa kunyonya, au ukwe kama baba mkwe, na anatakiwa awe muislamu aliyebaleghe, mwaminifu, kwani lengo la maharim ni kumlinda mwanamke na kumchunga na kumjali katika mambo yake.
  5. Sheria imempa kipaumbele mwanamke, na imemhami na kumlinda.
  6. Haikubaliki swala ya sunna isiyokuwa na sababu, baada ya swala ya Alfajiri na Lasiri, na haingii hapa kulipa swala ya faradhi iliyopita, na zenye sababu, kama salamu ya msikiti na mfano wake.
  7. Uharamu wa kusali mara tu baada ya kuchomoza Jua, bali ni lazima linyanyuke kiasi cha mkuki, kwa takribani kama dakika kumi (10) mpaka robo saa hivi.
  8. Wakati wa Lasiri unakwenda mpaka kuzama Jua.
  9. Ndani ya hadithi kuna kufaa kufunga safari kwenda katika misikiti mitatu.
  10. Fadhila na ubora wa misikiti mitatu, na tofauti yake kwa misikiti mingine.
  11. Hairuhusiwi kusafiri kwenda kufanya ziara ya makaburi, hata kama ni kaburi la Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, ila inafaa kulitembelea kwa anayeishi Madina, au akalifikia kwa lengo la kisheria au lengo linalofaa.
Ziada