عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما مرفوعاً: «الدنيا متاع، وخير متاعها المرأة الصالحة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillahi bin Amriy bin Aaswi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Dunia ni starehe, na starehe yake bora ni mke mwema".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Dunia kwa yale yaliyomo ni kitu cha kustarehesha kwa muda kisha kinatoweka, lakini starehe bora ya hii dunia yenye kuondoka ni mke mwema, anayesaidia kuipata Akhera, na amefafanua Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kwa kauli yake kuwa: "Akimtazama anamfurahisha, na akimuamrisha anamtii, na akiwa mbali naye anamuhifadhi katika nafsi yake na mali yake".