عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «لاَ يَفْرَك مُؤْمِنٌ مُؤْمِنَة إِنْ كَرِه مِنْهَا خُلُقًا رَضِيَ مِنْهَا آخَر»، أو قال: «غَيرُه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hachukii muumini wa kiume tabia za muumini wa kike, akichukia tabia fulani basi ataridhishwa na tabia nyingine". Au alisema: "tofauti na hiyo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Hadithi ya Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Hachukii muumini wa kiume tabia za muumini wa kike, akichukia tabia fulani basi ataridhishwa na tabia nyingine" Maana yake: hamchukii kwasababu ya tabia zake, na hata kama akichukia kwake tabia fulani basi ataridhia kwake tabia nyingine. Kumchukia: Inamaanisha ni chuki na uadui, yaani hamfanyii uadui muumini wa kiume muumini wa kike, kama mke wake kwa mfano, hamfanyii uadui na hamchukii pale anapoona kwake anayoyachukia katika tabia fulani, na hii ni kwasababu ni lazima kwa mwanadamu kusimamia uadilifu, na achunge namna ya kuishi naye kulingana na hali, na uadilifu na alinganishe kati ya mabaya na mazuri, na atazame ni yapi mengi na ni yapi yanayotokea kwa wingi, yatakayokuwa mengi na makubwa ndio yazidi kuleta athari, Huu ndio uadilifu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama