عن حذيفة بن اليمان رضي الله عنهما قال: «كنتُ مع النبي صلى الله عليه وسلم فبَالَ، وتوَضَّأ، ومَسَح على خُفَّيه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Hudhaifa bin Yamani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akaenda haja ndogo, akatawadha, na akafuta juu ya khufu zake (viatu vya ngozi mfano wa soksi)".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Anaeleza Hudhaifa bin Yamani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakuwa yeye alikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- , na hii ilikuwa katika mji wa Madina, akataka Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akidhi haja yake, akaenda mahala pa kutupa uchafu kwa watu fulani nyuma ya ukuta, akakidhi haja ndogo na akatawadha na akafuta juu ya khufu zake, na ulikuwa udhu wake huo ni baada ya kustanji kwa mawe, kama ilivyo ada yake -Rehema na Amani ziwe juu yake-.