+ -

عَنْ إِبرَاهِيمَ النَّخَعِيِّ عَنْ هَمَّامِ بنِ الحَارِثِ قَالَ:
بَالَ جَرِيرٌ، ثُمَّ تَوَضَّأَ، وَمَسَحَ عَلَى خُفَّيْهِ، فَقِيلَ: تَفْعَلُ هَذَا؟ فَقَالَ: نَعَمْ، رَأَيْتُ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ بَالَ، ثُمَّ تَوَضَّأَ وَمَسَحَ عَلَى خُفَّيْهِ. قَالَ الأَعْمَشُ: قَالَ إِبْرَاهِيمُ: كَانَ يُعْجِبُهُمْ هَذَا الحَدِيثُ؛ لِأَنَّ إِسْلَامَ جَرِيرٍ، كَانَ بَعْدَ نُزُولِ المَائِدَةِ.

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 272]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ibrahim Nakhai kutoka kwa Hammamu bin Harithi amesema:
Alikwenda haja ndogo Jariri kisha akatia udhu, na kafuta juu ya khufu zake, wakasema: Kwa nini unafanya hivi? Akasema: Ndio, Nilimuona Mtume rehema na amani ziwe juu yake, alikidhi haja ndogo, kisha akatia udhu na kafuta juu ya khufu zake. Amesema A'mashi: Amesema Ibrahimu: Ilikuwa ikiwashangaza sana hadithi hii; kwa sababu kusilimu kwa Jariri kulikuwa baada ya kuteremka Suratul-Maaida.

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 272]

Ufafanuzi

Alikidhi haja ndogo Jariri bin Abdillah radhi za Allah ziwe juu yake kisha akatawadha, na akatosheka na kufuta juu ya khofu zake na hakuosha miguu yake, wakasema kumwambia walioko nao: Mbona unafanya hivi?! Akasema: Ndio, nilimuona Mtume rehema na amani ziwe juu yake, alikidhi haja ndogo, kisha akatawadha na akafuta juu ya khofu zake. Na Jariri alisilimu kwa kuchelewa baada ya kuteremka kwa suratul-Maaida ambayo ndani yake ina aya ya udhu, akiashiria kuwa kufuta juu ya khufu hakukufutwa kwa aya hiyo.

Katika Faida za Hadithi

  1. Pupa ya Maswahaba na wanafunzi wao ya kufuata sunna ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
  2. Amesema Nawawi: Wamekubaliana wanaozingatiwa makubaliano yao juu ya kufaa kufuta juu ya khufu mbili, safarini na nyumbani, sawa sawa iwe kwa haja au bila haja, mpaka inafaa kwa mwanamke alioko nyumbani kwake na mgonjwa asiyeweza kutembea.
  3. Ubora wa Jariri bin Abdillah radhi za Allah ziwe juu yake, kiasi kwamba alikuwa na kifua kipana, akistahamili kukemewa na wanafunzi wake, hata kama wamekosea katika hilo.
  4. Kumjibu mwenye kukataa kufuta juu ya khufu mbili na akadai kuwa kulifutwa; kwa sababu hadithi ya Jariri radhi za Allah ziwe juu yake imechelewa kuliko aya ya udhu.
  5. Kumebainishwa kwamba ni lazima kwa mwenye kukemewa jambo na akawa akiitakidi usahihi wake asimkasirikie anayemkemea, bali ajadiliane naye kulingana na dhana yake, bali ambainishie hoja yake katika hilo kwa majibu mazuri.
  6. Kutoa ushihidi kupitia historia wakati wa haja ya kufanya hivyo.
Tafsiri: Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kivetenamu Kikurdi Kireno Thai Kiassam الهولندية الدرية المجرية الجورجية المقدونية
Kuonyesha Tarjama