عن المغيرة بن شعبة رضي الله عنه قال: ((كُنت مع النبيَّ -صلَّى الله عليه وسلَّم- في سَفَر، فأهْوَيت لِأَنزِع خُفَّيه، فقال: دَعْهُما؛ فإِنِّي أدخَلتُهُما طَاهِرَتَين، فَمَسَح عليهما)).
[صحيح] - [متفق عليه، واللفظ للبخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Mughira bin Shu'ba -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: (Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika safari, nikanyoosha mikono ili nimvue viatu vyake (khufu), akasema; ziache; kwani hakika mimi nimezivaa zikiwa safi, akafuta juu yake).
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy na Muslim na tamko ni la Bukhaariy

Ufafanuzi

Alikuwa Mughira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika moja ya safari zake -Nayo ni safari yake katika vita vya Tabuk-, Alipoanza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake kutawadha, na akaosha uso wake na mikono yake, na akafuta kichwa chake, aliinama Mughira katika khufu za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ili azivue; kwaajili ya kuosha miguu miwili, Akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ziache na wala usizivue, kwani hakika mimi nimeingiza miguu yangu katika khufu hizi mbili na mimi nikiwa msafi, akafuta Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake juu ya khufu (viatu mfano wa soksi) mbili badala ya kuosha miguu miwili. Na hivyo hivyo soksi na mfano wake zinachukua hukumu ya khufu mbili.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama