+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضيَ اللهُ عنه:
أَنَّهُ لَقِيَهُ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي طَرِيقٍ مِنْ طُرُقِ الْمَدِينَةِ وَهُوَ جُنُبٌ، فَانْسَلَّ فَذَهَبَ فَاغْتَسَلَ، فَتَفَقَّدَهُ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَلَمَّا جَاءَهُ قَالَ: «أَيْنَ كُنْتَ يَا أَبَا هُرَيْرَةَ؟» قَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ، لَقِيتَنِي وَأَنَا جُنُبٌ فَكَرِهْتُ أَنْ أُجَالِسَكَ حَتَّى أَغْتَسِلَ، فَقَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «سُبْحَانَ اللهِ، إِنَّ الْمُؤْمِنَ لَا يَنْجُسُ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 371]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-:
Ya kwamba alikutana na Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika barabara miongoni mwa barabara za mji wa Madina huku akiwa na janaba, akamkwepa na akaenda kuoga, Mtume rehema na amani ziwe juu yake akamtafuta hakumpata, alipomjia akasema: "Ulikuwa wapi ewe Abuu Huraira?" Akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ulikutana nami, nami nikiwa na janaba, sikufurahishwa kukaa na wewe mpaka nioge, akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Sub-haana llaah, ametakasika Mwenyezi Mungu, hakika muumini hanajisiki".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 371]

Ufafanuzi

Alikutana Mtume rehema na amani ziwe juu yake na Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake katika baadhi ya njia za Madina, na Abuu Huraira alikuwa na janaba, na kwa sababu ya kumuheshimu kwake Mtume rehema na amani ziwe juu yake alichukia kukaa naye na kuzungumza naye hali yakuwa yuko katika hali ile, kwa kudhani kwake kuwa yeye ni najisi, akaenda kwa uficho na akaoga, kisha akarejea na akakaa, Mtume rehema na amani ziwe juu yake akamuuliza kuwa alikwenda wapi? Akamueleza kuhusu hali yake, na kwamba yeye alichukia kukaa naye hali yakuwa yeye ni najisi kwa sababu ya janaba, Mtume rehema na amani ziwe juu yake akastaajabu, na akasema: Hakika muumini ni msafi na wala hanajisiki kwa hali yoyote; akiwa hai na hata wakiwa maiti.

Katika Faida za Hadithi

  1. Janaba linamzuia mtu kuswali na kugusa msahafu na kukaa msikitini, na wala halizuii kukaa pamoja na Waislamu na kukutana nao, na wala mwenye janaba hawi najisi.
  2. Usafi wa muumini akiwa hai au maiti.
  3. Kuwaheshimu watu wenye heshima, na elimu, na utengefu, na kukaa nao kwa muonekano mzuri.
  4. Hapa kuna sheria ya mfuasi kumuomba idhini ya kuondoka anayemfuata, kwani Mtume rehema na amani ziwe juu yake alimkemea Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwa kuondoka kwake pasina yeye kujua, na hii ni kwa sababu kuomba ruhusa ni katika adabu nzuri.
  5. Kusema: Sub-haana llaah, ametakasika Mwenyezi Mungu, wakati wa kustaajabu.
  6. Kufaa mtu kusimulia mambo yake binafsi katika yale ya aibu, kwa ajili ya masilahi.
  7. Kafiri ni najisi, lakini najisi yake si ya kuonekana, kwa sababu ya uchafu wa itikadi yake.
  8. Amesema Nawawi: Na katika hadithi hii pia kuna adabu, ya kwamba msomi atakapoona kwa anayemfuata jambo analohofia kwake kwenda kinyume na usahihi basi amuulize, na amwambie lililo sahihi, na ambainishie hukumu yake, na Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi zaidi.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam الرومانية المجرية الجورجية
Kuonyesha Tarjama