+ -

عن عَبْدِ اللهِ بْنِ عُمَرَ رضي الله عنهما قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ:
«‌مَنْ ‌جَاءَ ‌مِنْكُمُ ‌الْجُمُعَةَ فَلْيَغْتَسِلْ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 894]
المزيــد ...

kutoka kwa Abdullahi bin Omari -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema: Nilimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema:
"Atakayekuja miongoni mwenu kwa ajili ya Ijumaa basi na aoge".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 894]

Ufafanuzi

Anasisitiza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa atakayetaka kuja kwa ajili ya swala ya Ijumaa basi inapendeza kwake kuoga, mfano wa kuoga kwake josho la janaba.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Pashto Kiassam الأمهرية الهولندية الغوجاراتية Luqadda Oromaha
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Mkazo wa kuoga kwa ajili ya Ijumaa, nakuwa hilo ni sunna kwa muumini siku ya Ijumaa na ikiwa wakati anataka kwenda kuswali ndio bora zaidi.
  2. Kutilia manani swala la usafi na harufu nzuri ni katika tabia njema za muislamu na adabu zake, na amri inakuwa na mkazo zaidi wakati wa kukutana na watu na kukaa nao, hasa hasa katika mikusanyiko na swala za jamaa.
  3. Tamko katika hadithi linamuhusu mwenye uwajibu wa kuswali Ijumaa; kwa sababu yeye ndiye anayekwenda kuswali.
  4. Ni lazima kwa mwenye kwenda katika swala ya Ijumaa awe msafi, aoge ili harufu iondoke katika mwili wake na ajitie manukato, na ikiwa atatawadha pekee pia itatosha.