+ -

عن أبِي هُرَيرةَ رضي الله عنه أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلمَ قال:
«إذا قُلْتَ لِصَاحِبِكَ: أَنْصِتْ، يومَ الجمعةِ، والْإِمامُ يَخْطُبُ، فَقَدْ لَغَوْتَ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 851]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Utakapomwambia mwenzako: Nyamaza, siku ya Ijumaa, na imamu akihutubu, basi utakuwa umefanya mchezo".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 851]

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa katika adabu za wajibu kwa atakayehudhuria hotuba ya Ijumaa: Ni kunyamaza na kumsikiliza hatibu; ili mtu azingatie mawaidha, nakuwa atakayezungumza walau kwa jambo dogo, na imamu akihutubu, akasema kumwambia mwenzie: "Nyamaza" na "Sikiliza", basi zitakuwa zimempita fadhila za swala ya Ijumaa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية Luqadda yuruuba الليتوانية الدرية الصربية الصومالية Luqadda kiniya ruwadiga الرومانية التشيكية Luqadda malgaashka Kiitaliano Luqadda Oromaha Luqadda kinaadiga الأوكرانية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa mazungumzo wakati wa hotuba, hata kama ni kuzia uovu au kujibu salamu au kumuombea dua aliyepiga chafya.
  2. Anaondolewa katika katazo hili atayemsemesha imamu au imamu akamsemesha yeye.
  3. Inafaa kuzungumza kati ya hotuba mbili.
  4. Akitajwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- na imamu akiwa katika hotuba basi unatakiwa kumswalia kwa siri, na hivyo hivyo kuitikia dua.