عن أبي هُريرة رضي الله عنه مرفوعًا: «إذا قلتَ لصاحبك: أَنْصِتْ يوم الجمعة والإمام يَخْطُبُ، فقد لَغَوْتَ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie- Hadithi Marfu'u: "Utakaposema kumwambia mwenzio: Nyamaza siku ya ijumaa na Imamu ana hutubu, utakuwa umefanya mchezo.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Na katika alama kubwa za Ijumaa ni hotuba mbili, na katika malengo yake ni kuwakumbusha watu na kuwaelekeza, na katika Adabu za lazima kwa msikilizaji: ni kunyamaza ndani ya hotuba hizo mbili na kumsikiliza hatibu, ili azingatie mawaidha, na ndiyo maana alitahadharisha Mtume rehema na Amani zimfikie- kutokana na kuzungumza, hata kama ni kwa kitu kidogo, mfano kumkataza mwenzie asizungumze hata kwa neno: "Nyamaza" na atakayezungumza na imamu ana hutubu atakuwa kafanya mchezo, na atakosa fadhila za Ijumaa; kwasababu atakuwa kaleta kinachomshughulisha na kumshughulisha mwingine kutosikiliza hotuba.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuna ulazima wa kunyamaza kwaajili ya hatibu siku ya Ijumaa, na wamekubaliana wanachuoni juu ya ulazima wa hilo.
  2. Uharamu wa kuzungumza wakati wa kusikiliza hotuba, na nikuwa hilo linavunja heshima ya mahala hapo, hata kama ni kukataza uovu na kujibu salamu, na kumjibu aliyepiga chafya, na kila kitakachofanya kuwasemesha wengine.
  3. Na inavuliwa katika hili, yule atakaye msemesha Imamu au imamu akamsemesha yeye.
  4. Na wamemvua wanachuoni yule atakayekuwa hamsikii hatibu kwasababu ya umbali, basi halazimiki kunyamaza bali ashughulike na kusoma na kufanya dhikri, ama asiyemsikia kwasababu ya uziwi, hatakiwi kumshughulisha aliyepembezoni mwake kwa kudhihirisha kisomo, na liwe hilo kati yake na nafsi yake.
  5. Adhabu ya mwenye kuzungumza ni kunyimwa fadhila za Ijumaa.
  6. Ruhusa ya kuongea kati ya hotuba mbili.
  7. Atakapotajwa Mtume rehema na Amani zimfikie na Imamu ana hutubu, unatakiwa kumtakia sala na salamu na kuitikia dua kwa siri, na litakuwa hilo kwako, ni kuzifanyia kazi hadithi.
Ziada